Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mathayo 19:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Yesu akawaambia: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, Katika uumbaji-mpya Mwana wa binadamu atakapoketi juu ya kiti chake cha ufalme chenye utukufu, ninyi ambao mmenifuata mtaketi pia juu ya viti vya ufalme kumi na viwili, mkiyahukumu yale makabila kumi na mawili ya Israeli.+

  • Luka 22:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 nami ninafanya agano pamoja nanyi, sawa na vile Baba yangu alivyofanya agano+ pamoja nami, kwa ajili ya ufalme,+

  • Ufunuo 1:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 naye alitufanya tuwe ufalme,+ makuhani+ kwa Mungu na Baba yake—ndiyo, kwake yeye na kuwe utukufu na nguvu milele.+ Amina.

  • Ufunuo 3:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Yeye atakayeshinda+ nitampa ruhusa ya kuketi pamoja nami katika kiti changu cha ufalme,+ kama vile nilivyoshinda na kuketi+ pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha ufalme.+

  • Ufunuo 5:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 nawe ukawafanya kuwa ufalme+ na makuhani+ kwa Mungu wetu,+ nao watatawala wakiwa wafalme+ juu ya dunia.”

  • Ufunuo 20:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Nami nikaona viti vya ufalme,+ na kulikuwa na wale walioketi juu yake, nao wakapewa mamlaka ya kuhukumu.+ Ndiyo, niliona nafsi za wale waliouawa kwa shoka kwa ajili ya ushahidi waliotoa kumhusu Yesu na kwa ajili ya kusema juu ya Mungu, na wale ambao hawakumwabudu yule mnyama-mwitu+ wala sanamu+ yake na ambao hawakupokea ile alama juu ya paji la uso wao na juu ya mkono wao.+ Nao wakawa hai na kutawala wakiwa wafalme+ pamoja na Kristo kwa miaka elfu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki