17 “Usiitamani nyumba ya mwenzako. Usimtamani mke wa mwenzako,+ wala mtumwa wake wala kijakazi wake wala ng’ombe-dume wake wala punda wake wala chochote cha mwenzako.”+
2 Kwa hiyo Ahabu akamwambia Nabothi: “Nipe+ shamba lako la mizabibu,+ ili liwe bustani+ yangu ya mboga,+ kwa maana liko karibu na nyumba yangu; nami nitakupa mahali pake shamba la mizabibu lililo bora kuliko hilo. Au ikiwa vema machoni pako,+ nitakupa pesa kama bei yake.”
11 Tafadhali, warudishieni leo mashamba yao,+ mizabibu yao, mizeituni na nyumba zao, na kiasi cha sehemu moja kwa mia cha pesa na nafaka, divai mpya na mafuta mnachowatoza kama faida.”
8 Ole wao wanaounganisha nyumba na nyumba,+ na wale wanaounganisha shamba na shamba hata nafasi isiwepo tena+ nanyi mmefanywa mkae peke yenu kabisa katikati ya nchi!
29 Watu wa nchi wenyewe wameendesha mbinu ya kupunja+ nao wamenyakua katika unyang’anyi,+ nao wamemtendea vibaya+ anayeteseka na aliye maskini, na kumpunja bila haki mkaaji mgeni.’+