17 “Usiitamani nyumba ya mwenzako. Usimtamani mke wa mwenzako,+ wala mtumwa wake wala kijakazi wake wala ng’ombe-dume wake wala punda wake wala chochote cha mwenzako.”+
21 “‘Wala usimtamani mke wa mwenzako.+ Wala usitamani kwa uchoyo nyumba ya mwenzako, shamba lake au mtumishi wake au kijakazi wake, ng’ombe wake au punda wake au kitu chochote cha mwenzako.’+
15 Ndipo akawaambia: “Endeleeni kufungua macho yenu na mjilinde na kila namna ya tamaa,+ kwa sababu hata wakati mtu ana vitu vingi uzima wake hautokani na vitu alivyo navyo.”+
7 Basi, tuseme nini? Je, Sheria ni dhambi?+ Isiwe hivyo kamwe! Kwa kweli singejua dhambi+ kama isingekuwa kwa sababu ya Sheria; na, kwa mfano, mimi singejua tamaa+ kama Sheria haingesema: “Usitamani.”+
14 Wana macho yenye kujaa uzinzi+ na yasiyoweza kuachana na dhambi,+ nao huzishawishi nafsi zisizo imara. Wana moyo uliozoezwa kutamani.+ Wao ni watoto waliolaaniwa.+