10 Haitazimwa wakati wa mchana wala wakati wa usiku; moshi wake utaendelea kupaa mpaka wakati usio na kipimo.+ Atakauka kutoka kizazi hata kizazi;+ milele na milele hakuna atakayevuka katikati yake.+
20 Kwa hiyo sikieni shauri la Yehova ambalo ametunga juu ya Edomu,+ na mawazo yake ambayo amefikiri juu ya wakaaji wa Temani:+ Hakika wadogo wa kundi watakokotwa huku na huku. Hakika kwa sababu yao atayafanya makao yao kuwa ukiwa.+
13 kwa hiyo Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Pia nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu+ na kukatilia mbali kutoka kwake mwanadamu na mnyama wa kufugwa,+ nami nitapafanya kuwa ukiwa kutoka Temani,+ mpaka Dedani.+ Wataanguka kwa upanga.
3 Nawe utaliambia, ‘Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova amesema hivi: “Mimi hapa niko dhidi yako, Ee eneo lenye milima la Seiri,+ nami nitaunyoosha mkono wangu juu yako+ na kukufanya uwe mahame, naam, kuwa ukiwa.+
19 Nayo Misri itakuwa mahame yenye ukiwa;+ nayo Edomu itakuwa nyika ya mahame yenye ukiwa,+ kwa sababu ya jeuri kwa wana wa Yuda, ambao walimwaga damu isiyo na hatia katika nchi yao.+