26 Walipokuwa wakiendelea kula, Yesu alichukua mkate+ na, baada ya kutoa baraka, akaumega,+ akawapa wanafunzi, akasema: “Chukueni, mle. Huu unamaanisha mwili wangu.”+
19 Pia, akachukua mkate,+ akashukuru, akaumega, akawapa, akisema: “Huu unamaanisha mwili+ wangu ambao utatolewa kwa ajili yenu.+ Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka mimi.”+
16 Kikombe+ cha baraka ambacho tunabariki, je, hicho si kushiriki katika damu ya Kristo? Ule mkate ambao tunamega,+ je, huo si kushiriki katika mwili wa Kristo?+
24 na, baada ya kutoa shukrani, akaumega+ na kusema: “Huu unamaanisha mwili+ wangu ambao ni kwa ajili yenu. Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka+ mimi.”