35 Kwa maana yeyote yule anayetaka kuiokoa nafsi yake ataipoteza; lakini yeyote yule anayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya habari njema ataiokoa.+
24 Hata hivyo, siifanyi nafsi yangu kuwa kitu chenye thamani sana kwangu,+ kama tu ningepata kumaliza mwendo+ wangu na huduma+ niliyopokea+ kutoka kwa Bwana Yesu, kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fadhili zisizostahiliwa za Mungu.+
10 Usiogope mateso ambayo yanakaribia kukupata.+ Tazama! Ibilisi+ ataendelea kuwatupa gerezani baadhi yenu ili mjaribiwe kwa ukamili,+ na ili muwe na dhiki+ siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufikia kifo,+ nami nitakupa taji la uzima.+