Zaburi Muziki wa Asafu. 82 Mungu amesimama katika kusanyiko+ la Mungu;+Anahukumu katikati ya miungu:+ 2 “Mtaendelea kuhukumu bila haki mpaka wakati gani+Na kuonyesha ubaguzi kwa waovu?+ Sela. 3 Iweni waamuzi kwa ajili ya mtu wa hali ya chini na mvulana asiye na baba.+Kwa mtu mwenye kuteseka na maskini, mtendeeni haki.+ 4 Okoeni mtu wa hali ya chini na maskini;+Wakomboeni kutoka katika mkono wa waovu.”+ 5 Hawajajua, wala hawaelewi;+Wanaendelea kutembea huku na huku katika giza;+Misingi yote ya dunia inatikiswa.+ 6 “Mimi mwenyewe nimesema, ‘Ninyi ni miungu,+Nanyi nyote ni wana wa Aliye Juu Zaidi.+ 7 Hakika mtakufa kama wanadamu;+Nanyi mtaanguka kama yeyote kati ya wakuu!’”+ 8 Usimame, Ee Mungu, uihukumu dunia;+Kwa maana wewe mwenyewe unapaswa kuyamiliki mataifa yote.+