Zekaria
7 Tena ikawa kwamba katika mwaka wa nne wa Mfalme Dario+ neno la Yehova lilimjia Zekaria, siku ya nne ya mwezi wa tisa, yaani, mwezi wa Kislevu.+ 2 Na watu wa Betheli wakawatuma Shareza na Regem-meleki na watu wake ili kuutuliza+ uso wa Yehova, 3 na kuwaambia makuhani+ wa nyumba ya Yehova wa majeshi, na manabii, wakisema: “Je, nilie mwezi wa tano,+ na kufunga, kama ambavyo nimefanya miaka hii mingi iliyopita?”+
4 Na neno la Yehova wa majeshi likaendelea kunijia, na kusema: 5 “Waambie watu wote wa nchi na makuhani, ‘Mlipofunga+ na kuomboleza katika mwezi wa 5 na mwezi wa 7,+ mkafanya hivyo kwa miaka 70,+ je, kweli mlifunga kwa ajili yangu mimi?+ 6 Na wakati mlikula na wakati mlikunywa, je, si ninyi mliokula, na je, si ninyi mliokunywa? 7 Je, haiwapasi kutii maneno+ ambayo Yehova alisema kupitia manabii wa kale,+ wakati Yerusalemu lilipokuwa na watu, likistarehe, pamoja na majiji yake yenye kulizunguka pande zote, na watu walipokuwa wakikaa Negebu+ na Shefela?’ ”+
8 Nalo neno la Yehova likaendelea kumjia Zekaria, na kusema: 9 “Yehova wa majeshi amesema hivi, ‘Fanyeni hukumu kwa haki ya kweli;+ na mtendeane kwa fadhili zenye upendo+ na rehema;+ 10 wala msimpunje mjane+ yeyote na mvulana yeyote asiye na baba,+ wala mkaaji mgeni+ au mwenye kuteseka,+ wala msipangiane jambo lolote baya mioyoni mwenu.’+ 11 Lakini waliendelea kukataa kusikiliza,+ nao wakaendelea kugeuza bega kwa ukaidi,+ wakafanya masikio yao kuwa magumu mno yasiweze kusikia.+ 12 Nayo mioyo yao+ wakaifanya kuwa kama jiwe gumu ili isitii sheria+ na maneno ambayo Yehova wa majeshi alipeleka kwa roho yake,+ kupitia manabii wa kale;+ hata Yehova wa majeshi akakasirika sana.”+
13 “ ‘Basi ikawa kwamba, kama vile alivyoita wala hawakusikiliza,+ vivyo hivyo wao waliita na mimi sikusikiliza,’+ Yehova wa majeshi amesema. 14 ‘Ndipo nikawatupa kama tufani kotekote katika mataifa+ yote ambayo hawakuyajua;+ nayo nchi imeachwa ukiwa nyuma yao, bila kuwa na mtu yeyote anayepita kati yake wala anayerudi;+ nao wakaifanya nchi yenye kutamanika+ kuwa kitu cha kushangaza.’ ”