Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 11:46, 47
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 46 “‘Hiyo ndiyo sheria kuhusu wanyama, ndege, kila kiumbe anayeishi majini, na kila kiumbe anayetambaa, 47 ili kutofautisha viumbe walio safi na wasio safi na viumbe wanaoweza kuliwa na wasioweza kuliwa.’”+

  • Kumbukumbu la Torati 14:4-20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Hawa ndio wanyama mnaoweza kula:+ ng’ombe, kondoo, mbuzi, 5 paa, swala, kulungu, mbuzi mwitu, mbawala, kondoo mwitu, na kondoo wa mlimani. 6 Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizopasuka na zilizogawanyika mara mbili na ambaye anacheua. 7 Lakini hampaswi kuwala wanyama wafuatao wanaocheua au wenye kwato zilizogawanyika: ngamia, sungura, na wibari, kwa sababu wanacheua lakini kwato zao hazijapasuka. Wao si safi kwenu.+ 8 Pia, msimle nguruwe kwa sababu ana kwato zilizopasuka lakini hacheui. Yeye si safi kwenu. Msile kamwe nyama yao wala kugusa mizoga yao.

      9 “Kati ya viumbe wote wanaoishi ndani ya maji, mnaweza kula wafuatao: Mnaweza kumla kiumbe yeyote mwenye mapezi na magamba.+ 10 Lakini hampaswi kumla kiumbe yeyote ambaye hana mapezi na magamba. Yeye si safi kwenu.

      11 “Mnaweza kumla ndege yeyote aliye safi. 12 Lakini hampaswi kuwala ndege wafuatao: tai, furukombe, tumbusi mweusi,*+ 13 mwewe mwekundu, mwewe mweusi, kila aina ya ndege mbua, 14 kila aina ya kunguru, 15 mbuni, bundi, shakwe, kila aina ya kipanga, 16 bundi mdogo, bundi mwenye masikio marefu, batamaji, 17 mwari, tumbusi, mnandi, 18 korongo, kila aina ya kulastara, hudihudi, na popo. 19 Pia, kila kiumbe* mwenye mabawa anayeishi katika makundi makubwa si safi kwenu. Hawapaswi kuliwa. 20 Mnaweza kumla kiumbe yeyote safi anayeruka.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki