Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 “Unapaswa kuleta katika nyumba yangu mimi, Yehova Mungu wako, mazao bora ya kwanza yaliyokomaa* ya ardhi yako.+

      “Usimchemshe mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.+

  • Hesabu 15:18, 19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 “Waambie hivi Waisraeli: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka 19 nanyi mle chakula chochote cha* nchi hiyo,+ mnapaswa kumtolea Yehova kiasi fulani kama mchango.

  • Hesabu 18:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Vitu hivi pia vitakuwa vyenu: zawadi ambazo Waisraeli wanatoa kuwa mchango+ pamoja na matoleo yao yote ya kutikiswa.+ Nimekupa wewe na wanao na mabinti wako vitu hivyo ili viwe posho yenu ya kudumu.+ Kila mtu aliye safi katika nyumba yako anaweza kula.+

  • Hesabu 18:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 “Unapaswa kuwaambia hivi Walawi: ‘Mtapokea kutoka kwa Waisraeli sehemu ya kumi ambayo nimewapa ninyi kutoka kwao ili iwe urithi wenu,+ nanyi mnapaswa kumtolea Yehova mchango wa sehemu ya kumi kutoka katika sehemu hiyo ya kumi.+

  • Hesabu 31:28, 29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Kutoka kwa wanajeshi walioenda vitani, mtachukua nafsi* moja kutoka kwa kila nafsi 500 za wanadamu, za ng’ombe, za punda, na kondoo ili iwe kodi ya Yehova. 29 Mnapaswa kuchukua nafsi hizo kutoka katika fungu lao na kumpa kuhani Eleazari kama mchango kwa Yehova.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki