Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 12:1-3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Yehova akamwambia Abramu: “Ondoka katika nchi yako na kutoka kwa watu wako wa ukoo na nyumba ya baba yako uende katika nchi nitakayokuonyesha;+ 2 Nitakufanya kuwa taifa kubwa, nami nitakubariki, nami nitalifanya jina lako liwe kuu, nawe utakuwa baraka.+ 3 Nitawabariki wale wanaokubariki, nami nitawalaani wale wanaokulaani,+ na familia zote duniani hakika zitabarikiwa* kupitia kwako.”+

  • Mwanzo 22:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Na malaika wa Yehova akamwita Abrahamu mara ya pili kutoka mbinguni,

  • Mwanzo 22:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 hakika nitakubariki, nami hakika nitaufanya uzao* wako uwe mwingi kama nyota za mbinguni na kama chembe za mchanga kwenye ufuo wa bahari,+ na uzao* wako utamiliki lango la* maadui wake.+

  • Mwanzo 26:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kaa kama mgeni katika nchi hii,+ nami nitaendelea kuwa pamoja nawe na kukubariki kwa sababu nitakupa wewe na uzao wako* nchi zote hizi,+ nami nitatimiza kiapo hiki nilichomwapia Abrahamu baba yako:+ 4 ‘Nitaufanya uzao* wako uwe mwingi kama nyota za mbinguni;+ nami nitaupa uzao* wako nchi zote hizi;+ na kupitia uzao* wako mataifa yote ya dunia yatajipatia baraka,’+

  • Kutoka 23:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Mnapaswa kunitumikia mimi, Yehova Mungu wenu,+ nami nitabariki mkate wenu na maji yenu.+ Nitaondoa magonjwa miongoni mwenu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki