-
Mambo ya Walawi 25:33, 34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Mlawi asipokomboa nyumba yake, nyumba hiyo iliyouzwa katika jiji la Walawi itarudishwa wakati wa Mwadhimisho wa Miaka 50,+ kwa sababu nyumba zilizo katika majiji ya Walawi ni urithi wao miongoni mwa Waisraeli.+ 34 Isitoshe, malisho+ yanayozunguka majiji yao hayapaswi kuuzwa, kwa sababu ni urithi wao wa kudumu.
-
-
Hesabu 35:2-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 “Waagize Waisraeli wawape Walawi majiji ya kuishi kutoka katika urithi watakaomiliki,+ nao wanapaswa kuwapa Walawi malisho yanayozunguka majiji hayo.+ 3 Wataishi katika majiji hayo, na malisho hayo yatakuwa ya mifugo yao, na ya mali zao, na wanyama wao wengine wote. 4 Malisho ya majiji mtakayowapa Walawi yatakuwa na upana wa mikono 1,000* kila upande kutoka kwenye ukuta wa jiji.
-