-
Yoshua 7:24-26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Yoshua na Waisraeli wote wakamchukua Akani+ mwana wa Zera, zile fedha, lile vazi rasmi maridadi, na kile kipande cha dhahabu,+ pamoja na wanawe, binti zake, ng’ombe dume wake, punda wake, kondoo na mbuzi wake, hema lake, na vitu vyake vyote, wakavileta katika Bonde la* Akori.+ 25 Yoshua akasema: “Kwa nini umetuletea msiba?*+ Leo Yehova atakuletea msiba.” Ndipo Waisraeli wote wakawapiga mawe,+ kisha wakawateketeza kwa moto.+ Naam, waliwapiga mawe wote. 26 Nao wakarundika mawe mengi juu yake ambayo yapo hadi leo. Ndipo hasira ya Yehova ikapoa.+ Ndiyo sababu tangu siku hiyo mahali hapo panaitwa Bonde la Akori.*
-