Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Samweli 8:15-18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Daudi akaendelea kutawala Israeli yote,+ naye aliwatawala watu wake wote+ kwa haki na uadilifu.+ 16 Yoabu+ mwana wa Seruya alikuwa mkuu wa jeshi, na Yehoshafati+ mwana wa Ahiludi alifanya kazi ya kuweka kumbukumbu. 17 Sadoki+ mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani, na Seraya alikuwa mwandishi. 18 Benaya+ mwana wa Yehoyada aliwasimamia Wakerethi na Wapelethi.+ Na wana wa Daudi walikuwa wahudumu wakuu.*

  • 2 Samweli 23:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Mungu wa Israeli alisema;

      Mwamba wa Israeli+ aliniambia:

      ‘Yule anayetawala wanadamu anapokuwa mwadilifu,+

      Anapotawala kwa kumwogopa Mungu,+

       4 Ni kama mwangaza wa asubuhi jua linapoangaza,+

      Asubuhi isiyo na mawingu.

      Ni kama mwangaza baada ya mvua kunyesha,

      Ambao unaotesha majani duniani.’+

  • Zaburi 78:70-72
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 70 Alimchagua Daudi+ mtumishi wake

      Na kumtoa katika mazizi ya kondoo,+

      71 Alimwondoa katika kazi ya kuchunga kondoo wanaonyonyesha;

      Akamfanya kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake,+

      Na wa Israeli, urithi wake.+

      72 Aliwachunga kwa utimilifu wa moyo,+

      Na kwa mikono stadi aliwaongoza.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki