Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 3:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 nitafanya uliloomba.+ Nitakupa moyo wenye hekima na uelewaji,+ hivi kwamba kama vile ambavyo hajawahi kamwe kuwapo mtu mwingine kama wewe kabla yako, hatawahi kamwe kuwapo mtu mwingine kama wewe baada yako.+

  • 1 Wafalme 4:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Naye Mungu akampa Sulemani hekima na utambuzi mwingi sana na moyo wenye uelewaji mwingi kama mchanga kwenye ufuo wa bahari.+

  • Ayubu 35:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Hutufundisha+ kuliko wanyama mwitu wa dunia,+

      Naye hutufanya tuwe na hekima kuliko ndege wa angani.

  • Methali 2:6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  6 Kwa maana Yehova mwenyewe hutoa hekima;+

      Na kinywani mwake hutoka ujuzi na utambuzi.

  • Mhubiri 2:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Yeye humpa mtu anayempendeza hekima na ujuzi na shangwe,+ lakini humpa mtenda dhambi kazi ya kukusanya na kurundika tu, ili ampe yule anayempendeza Mungu wa kweli.+ Hili pia ni ubatili, kukimbiza upepo.

  • Danieli 1:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Na Mungu wa kweli aliwapa vijana* hao wanne ujuzi na ufahamu wa kila aina ya maandishi na hekima; naye Danieli alipewa uwezo wa kuelewa maono na ndoto za kila aina.+

  • Mathayo 11:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Ndipo Yesu akasema: “Ninakusifu hadharani, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye elimu nawe umeyafunua kwa watoto wadogo.+

  • Yakobo 1:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Kwa hiyo, ikiwa yeyote kati yenu anakosa hekima, na aendelee kumwomba Mungu,+ kwa maana yeye huwapa wote kwa ukarimu na bila kushutumu,*+ naye atapewa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki