6Katika mwaka wa 480 baada ya Waisraeli* kutoka katika nchi ya Misri,+ mwaka wa nne baada ya Sulemani kuwekwa kuwa mfalme wa Israeli, mwezi wa Zivu*+ (yaani, mwezi wa pili), Sulemani alianza kujenga nyumba ya Yehova.*+
16Basi wakaliingiza Sanduku la Mungu wa kweli na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amepiga ili aliweke humo;+ nao wakatoa dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za ushirika mbele za Mungu wa kweli.+
14 Pia, Mfalme Koreshi alitoa katika hekalu la Babiloni vyombo vya dhahabu na fedha vya nyumba ya Mungu ambavyo Nebukadneza alikuwa amevichukua hekaluni huko Yerusalemu, na kuvileta katika hekalu la Babiloni.+ Alivikabidhi kwa mtu aitwaye Sheshbazari,*+ ambaye Koreshi alimteua kuwa gavana.+