Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yoshua 7:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Wakanaani na wakaaji wote wa nchi hii watakaposikia habari hii, watatuzingira na kufutilia mbali jina letu kutoka duniani, nawe utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?”+

  • 1 Samweli 12:22
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 22 Kwa ajili ya jina lake kuu,+ Yehova hatawaacha watu wake,+ kwa sababu Yehova ameamua mwenyewe kuwafanya ninyi kuwa watu wake.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 14:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Kisha Asa akamlilia Yehova Mungu wake+ akisema: “Ee Yehova, haijalishi kwako ikiwa wale unaowasaidia ni wengi au hawana nguvu.+ Tusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana tunakutegemea* wewe,+ na katika jina lako tumekuja kupigana na umati huu.+ Ee Yehova, wewe ni Mungu wetu. Usiache mwanadamu anayeweza kufa akushinde.”+

  • Zaburi 115:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 115 Usitutukuze sisi, Ee Yehova, usitutukuze sisi,*

      Bali litukuze jina lako+

      Kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu na uaminifu wako.+

       2 Kwa nini mataifa yaseme:

      “Yuko wapi Mungu wao?”+

  • Isaya 48:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  9 Lakini kwa sababu ya jina langu nitaizuia hasira yangu;+

      Kwa ajili ya sifa yangu mwenyewe nitajizuia,

      Nami sitakuangamiza.+

  • Yeremia 14:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Ingawa makosa yetu yanatushtaki,

      Ee Yehova, tenda kwa ajili ya jina lako.+

      Kwa maana matendo yetu ya ukosefu wa uaminifu ni mengi,+

      Nasi tumekutendea dhambi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki