Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 16:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Walipokuwa wakiingia, Samweli alimwona Eliabu+ na kusema: “Hakika mtiwa-mafuta wa Yehova amesimama hapa mbele zake.” 7 Lakini Yehova akamwambia Samweli: “Usitazame sura yake wala urefu wake,+ kwa maana nimemkataa. Kwa kuwa Mungu haoni kama mwanadamu anavyoona, kwa maana mwanadamu huona kinachoonekana kwa macho, lakini Yehova huona ndani ya moyo.”+

  • 1 Mambo ya Nyakati 28:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 “Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako na kumtumikia kwa moyo kamili*+ na kwa nafsi* yenye shangwe;* kwa maana Yehova huichunguza kabisa mioyo yote,+ naye hutambua kila mwelekeo wa fikira.+ Ukimtafuta, atakuruhusu umpate,+ lakini ukimwacha, atakukataa milele.+

  • Zaburi 17:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Umeuchunguza moyo wangu, umenikagua wakati wa usiku;+

      Umenisafisha;+

      Utagundua kwamba sijapanga njama ya kutenda uovu wowote,

      Na kinywa changu hakijatenda dhambi.

  • Zaburi 139:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Nichunguze kabisa, Ee Mungu, uujue moyo wangu.+

      Nipime, uyajue mawazo yangu yanayonihangaisha.*+

  • Yeremia 20:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Lakini wewe, Ee Yehova wa majeshi, unamchunguza mwadilifu;

      Unaona mawazo ya ndani kabisa* na pia moyo.+

      Acha nione ukiwalipiza kisasi,+

      Kwa maana nimeileta kesi yangu kwako.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki