Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 1:29
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Kisha Mungu akasema: “Tazama nimewapa kila mmea duniani pote unaozaa mbegu na kila mti unaozaa matunda yenye mbegu. Itakuwa chakula chenu.+

  • Mwanzo 9:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kila mnyama aliye hai anayetembea anaweza kuwa chakula chenu.+ Kama nilivyowapa mimea, ninawapa hao wote wawe chakula chenu.+

  • Zaburi 144:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  3 Ee Yehova, mwanadamu ni nini hata umtambue,

      Mwana wa mtu anayeweza kufa ni nini hata umkazie uangalifu?+

  • Mathayo 6:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 “Kwa hiyo ninawaambia: Acheni kuhangaikia+ uhai wenu* kuhusu kile mtakachokula au kunywa, au juu ya miili yenu kuhusu kile mtakachovaa.+ Je, uhai* si zaidi ya chakula na mwili zaidi ya mavazi?+

  • Mathayo 6:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Basi, ikiwa Mungu huivika hivyo mimea ya shambani, ambayo ipo hapa leo na kesho hutupwa ndani ya jiko, je, hatawavika vizuri zaidi ninyi wenye imani ndogo?

  • Yohana 3:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 “Kwa maana, Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa pekee,+ ili kila mtu anayemwamini* asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.+

  • Matendo 14:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 ingawa hakujiacha bila ushahidi+ kwa kuwa alitenda mema, akiwapa ninyi mvua kutoka mbinguni na majira ya mavuno,+ akiwashibisha kwa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha.”+

  • Waebrania 2:6-8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Lakini mahali fulani shahidi mmoja alisema: “Mwanadamu ni nini hivi kwamba unamweka akilini, au mwana wa mtu hivi kwamba unamtunza?+ 7 Ulimfanya awe mdogo kidogo kuliko malaika; ulimvika taji kwa utukufu na heshima, na kumweka juu ya kazi za mikono yako. 8 Ulivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake.”+ Kwa kuvitiisha vitu vyote chini yake,+ Mungu hakuacha kitu chochote kisichotiishwa chini yake.+ Ingawa hivyo, bado hatuoni vitu vyote vikiwa vimetiishwa chini yake.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki