-
2 Mambo ya Nyakati 34:20, 21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
20 Kisha mfalme akamwagiza hivi Hilkia, Ahikamu+ mwana wa Shafani, Abdoni mwana wa Mika, mwandishi Shafani, na Asaya mtumishi wa mfalme: 21 “Nendeni mkatafute ushauri wa Yehova kwa niaba yangu na kwa niaba ya watu ambao wamebaki Israeli na Yuda kuhusu maneno ya kitabu hiki ambacho kimepatikana; kwa maana ghadhabu ya Yehova itakayomwagwa dhidi yetu ni kali kwa sababu mababu zetu hawakutekeleza neno la Yehova kwa kuyashika mambo yote yaliyoandikwa katika kitabu hiki.”+
-
-
Yeremia 39:13, 14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
13 Basi Nebuzaradani mkuu wa walinzi, Nebushazbani yule Rabsarisi,* Nergal-shareza yule Rabmagi,* na wakuu wote wa mfalme wa Babiloni wakawatuma watu 14 wamtoe Yeremia katika Ua wa Walinzi+ na kumkabidhi kwa Gedalia+ mwana wa Ahikamu+ mwana wa Shafani+ ili apelekwe nyumbani kwake. Basi akaishi pamoja na watu wengine.
-