Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 14:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Ndipo nikasema: “Ole wangu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova! Tazama, manabii wanawaambia, ‘Hamtaona upanga, wala hamtakumbwa na njaa kali, bali nitawapa amani ya kweli mahali hapa.’”+

  • Yeremia 23:16, 17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Yehova wa majeshi anasema hivi:

      “Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowatabiria ninyi.+

      Wanawadanganya.*

      Wanasema maono ya moyo wao wenyewe,+

      Si kutoka katika kinywa cha Yehova.+

      17 Wanawaambia tena na tena wale wasioniheshimu,

      ‘Yehova amesema hivi: “Mtakuwa na amani.”’+

      Nao wanamwambia kila mtu anayefuata moyo wake mkaidi,

      ‘Hutapatwa na msiba wowote.’+

  • Yeremia 27:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Msiyasikilize maneno ya manabii wanaowaambia, ‘Hamtamtumikia mfalme wa Babiloni,’+ kwa sababu wanawatabiria uwongo.+

  • Yeremia 28:1, 2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Mwaka huohuo, mwanzoni mwa utawala wa Mfalme Sedekia+ wa Yuda, katika mwaka wa nne, mwezi wa tano, nabii Hanania mwana wa Azuri kutoka Gibeoni+ aliniambia hivi katika nyumba ya Yehova mbele ya makuhani na watu wote: 2 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi, ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babiloni.+

  • Maombolezo 2:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Maono ambayo manabii wako waliona kwa ajili yako yalikuwa ya uwongo na yasiyofaa kitu,+

      Nao hawakufunua kosa lako ili kuzuia usipelekwe utekwani,+

      Bali waliendelea kukupa maono yenye ujumbe wa uwongo na unaopotosha.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki