10 “Nawe, mtumishi wangu Yakobo, usiogope,” asema Yehova,
“Wala usihofu, Ee Israeli.+
Kwa maana nitakuokoa kutoka mbali
Na uzao wako kutoka katika nchi waliyopelekwa utekwani.+
Yakobo atarudi na kuwa na utulivu bila usumbufu,
Na hakuna yeyote atakayewaogopesha.”+
11 “Kwa maana mimi niko pamoja nawe,” asema Yehova, “ili nikuokoe.
Lakini nitaleta maangamizi katika mataifa yote ambako nilikutawanya;+
Lakini wewe, sitakuangamiza.+
Nitakutia nidhamu kwa kiwango kinachofaa,
Nami sitakuacha kamwe bila kukuadhibu.”+