3 Yehova anasema hivi: “Tekelezeni haki na uadilifu. Na mtu anayenyang’anywa, mwokoeni kutoka mikononi mwa mtu laghai. Msimtese mkaaji yeyote mgeni, na msimdhuru yatima yeyote au mjane.+ Nanyi msimwage damu yoyote isiyo na hatia mahali hapa.+
16 “‘Haya ndiyo mambo mnayopaswa kufanya: Kila mtu amwambie mwenzake ukweli,+ na hukumu mnazotoa katika malango yenu zinapaswa kutetea ukweli na amani.+