3 Yehova anasema hivi: “Tekelezeni haki na uadilifu. Na mtu anayenyang’anywa, mwokoeni kutoka mikononi mwa mtu laghai. Msimtese mkaaji yeyote mgeni, na msimdhuru yatima yeyote au mjane.+ Nanyi msimwage damu yoyote isiyo na hatia mahali hapa.+
9 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Imetosha, enyi viongozi wa Israeli!’
“‘Acheni ukatili na ukandamizaji, na mtende mambo ya haki na ya uadilifu.+ Acheni kuchukua kwa nguvu mali ya watu wangu,’+ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.