-
Yeremia 43:10, 11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
10 Kisha uwaambie, ‘Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: “Tazameni, ninamwita Nebukadneza* mfalme wa Babiloni, mtumishi wangu,+ nami nitakiweka kiti chake cha ufalme juu ya mawe haya ambayo nimeyaficha, naye atalitandaza hema lake la kifalme juu yake.+ 11 Naye ataingia na kuipiga nchi ya Misri.+ Yeyote aliyekusudiwa kufa kwa ugonjwa hatari atakufa kwa ugonjwa hatari, na yeyote aliyekusudiwa kwenda utekwani ataenda utekwani, na yeyote aliyekusudiwa kufa kwa upanga atakufa kwa upanga.+
-
-
Yeremia 46:25, 26Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
25 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Sasa ninamkazia fikira Amoni+ kutoka No,*+ Farao, Misri, miungu yake,+ wafalme wake—naam, Farao na wote wanaomtumaini.’+
26 “‘Nami nitawatia mikononi mwa wale wanaotaka kuwaua, mikononi mwa Mfalme Nebukadneza* wa Babiloni+ na watumishi wake. Lakini baadaye watu watakaa ndani yake kama zamani,’ asema Yehova.+
-