Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 15:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Nguvu zangu na uwezo wangu ni Yah,* kwa maana amekuwa wokovu wangu.+

      Huyu ni Mungu wangu, nitamsifu;+ Mungu wa baba yangu,+ nitamkweza.+

  • 1 Samweli 2:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Kisha Hana akasema hivi katika sala:

      “Moyo wangu unashangilia katika Yehova;+

      Pembe yangu imekwezwa* na Yehova.

      Kinywa changu kimefunguliwa wazi dhidi ya maadui wangu,

      Kwa maana ninashangilia kwa sababu ya matendo yako ya wokovu.

  • Zaburi 18:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 Yehova ni jabali langu na ngome yangu na Mwokozi wangu.+

      Mungu wangu ni mwamba wangu,+ ninayemkimbilia,

      Ngao yangu na pembe* yangu ya wokovu,* kimbilio langu salama.*+

  • Zaburi 27:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Yehova ni nuru yangu+ na wokovu wangu.

      Nimwogope nani?+

      Yehova ni ngome ya uhai wangu.+

      Nimhofu nani?

  • Isaya 61:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Nitashangilia sana katika Yehova.

      Nafsi yangu yote itashangilia katika Mungu wangu.+

      Kwa maana amenivisha mavazi ya wokovu;+

      Amenifunika kwa joho* la uadilifu,

      Kama bwana harusi anayevaa kilemba kama cha kuhani,+

      Na kama bibi harusi anayejipamba kwa mapambo yake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki