-
Mathayo 12:9-14Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Baada ya kutoka hapo, akaingia ndani ya sinagogi lao, 10 na tazama! kulikuwa na mtu aliyepooza mkono!+ Basi, ili wapate sababu ya kumshtaki wakamuuliza, “Je, ni halali kumponya mtu siku ya Sabato?”+ 11 Akawaambia: “Ukiwa na kondoo mmoja, naye kondoo huyo atumbukie shimoni siku ya Sabato, je, kuna yeyote kati yenu ambaye hatamshika na kumtoa humo?+ 12 Kwa kweli, mwanadamu ni mwenye thamani sana kuliko kondoo! Basi ni halali kutenda mema siku ya Sabato.” 13 Kisha akamwambia mtu huyo: “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukawa mzima kama ule mkono mwingine. 14 Lakini Mafarisayo wakaenda nje na kupanga njama ili wamuue.
-
-
Luka 6:6-11Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
6 Siku nyingine ya Sabato+ aliingia katika sinagogi, akaanza kufundisha. Kulikuwa na mtu aliyepooza mkono wa kulia.+ 7 Waandishi na Mafarisayo walikuwa wakimwangalia Yesu kwa makini ili waone kama angeponya katika siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki. 8 Hata hivyo, alijua mawazo yao,+ basi akamwambia yule mtu aliyepooza mkono: “Inuka usimame hapa katikati.” Naye akainuka na kusimama hapo. 9 Kisha Yesu akawauliza: “Je, ni halali kufanya mema au kufanya mabaya siku ya Sabato, kuokoa uhai* au kuuangamiza?”+ 10 Baada ya kuwatazama wote waliokuwapo, Yesu akamwambia mtu huyo: “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukapona. 11 Lakini wakakasirika sana, wakaanza kushauriana kuhusu jambo ambalo wangemtendea Yesu.
-