Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Marko 3:1-6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Yesu akaingia tena ndani ya sinagogi, na palikuwa na mtu aliyepooza mkono.+ 2 Basi walikuwa wakimwangalia sana waone kama atamponya mtu huyo siku ya Sabato, ili wamshtaki. 3 Akamwambia yule mtu aliyepooza mkono: “Simama uje hapa katikati.” 4 Kisha akawauliza: “Je, ni halali kufanya mema au kufanya mabaya siku ya Sabato, kuokoa uhai* au kuua?”+ Lakini wakanyamaza. 5 Akawatazama kwa hasira na kuhuzunika sana kwa sababu mioyo yao ilikuwa migumu,+ akamwambia mtu huyo: “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha mkono wake, nao ukapona. 6 Ndipo Mafarisayo wakaenda nje na mara moja wakafanya mkutano pamoja na wafuasi wa chama cha Herode+ ili wamuue Yesu.

  • Luka 6:6-11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Siku nyingine ya Sabato+ aliingia katika sinagogi, akaanza kufundisha. Kulikuwa na mtu aliyepooza mkono wa kulia.+ 7 Waandishi na Mafarisayo walikuwa wakimwangalia Yesu kwa makini ili waone kama angeponya katika siku ya Sabato, ili wapate sababu ya kumshtaki. 8 Hata hivyo, alijua mawazo yao,+ basi akamwambia yule mtu aliyepooza mkono: “Inuka usimame hapa katikati.” Naye akainuka na kusimama hapo. 9 Kisha Yesu akawauliza: “Je, ni halali kufanya mema au kufanya mabaya siku ya Sabato, kuokoa uhai* au kuuangamiza?”+ 10 Baada ya kuwatazama wote waliokuwapo, Yesu akamwambia mtu huyo: “Nyoosha mkono wako.” Akaunyoosha, nao ukapona. 11 Lakini wakakasirika sana, wakaanza kushauriana kuhusu jambo ambalo wangemtendea Yesu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki