Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 7:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 na watu wangu ambao wameitwa kwa jina langu+ wakijinyenyekeza+ na kusali na kuutafuta uso wangu na kuacha njia zao ovu,+ ndipo nitakaposikia kutoka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na kuiponya nchi yao.+

  • Zaburi 32:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Mwishowe nikaungama dhambi yangu kwako;

      Sikufunika kosa langu.+

      Nilisema: “Nitaungama makosa yangu kwa Yehova.”+

      Nawe ukanisamehe kosa la dhambi zangu.+ (Sela)

  • Zaburi 51:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Dhidi yako wewe—wewe zaidi ya wote*—nimetenda dhambi;+

      Nimetenda yaliyo mabaya machoni pako.+

      Kwa hiyo, wewe ni mwadilifu unapoongea,

      Wewe ni mwenye haki katika hukumu yako.+

  • Methali 28:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Anayefunika makosa yake hatafanikiwa,+

      Lakini yeyote anayeyaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.+

  • Luka 18:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Lakini yule mkusanya kodi alikuwa amesimama mbali kidogo na hata hakutaka kutazama mbinguni, bali alijipigapiga kifuani akisema, ‘Ee Mungu, nihurumie* mimi mtenda dhambi.’+

  • 1 Yohana 1:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Tukiungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na mwadilifu naye atatusamehe dhambi zetu na kutusafisha ukosefu wote wa uadilifu.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki