Kwa kiongozi; juu ya Gitithi. Wa Asafu.+
81 Mshangilieni Mungu kwa sauti, nguvu zetu.+
Mpazieni sauti kwa ushindi Mungu wa Yakobo.
 2 Anzisheni muziki na kuchukua tari,
Kinubi chenye sauti tamu pamoja na kinanda.
 3 Pigeni pembe wakati wa mwezi mpya,+
Wakati wa mwezi mpevu, kwa ajili ya siku ya sherehe yetu.+
 4 Kwa maana ni agizo kwa Israeli,
Sheria ya Mungu wa Yakobo.+
 5 Aliiweka ili iwe kikumbusho kwa Yosefu+
Alipoenda kuishambulia nchi ya Misri.+
Nilisikia sauti ambayo sikuitambua:
 6 “Niliuinua mzigo kutoka begani mwake;+
Mikono yake iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
 7 Katika taabu uliita, nami nikakuokoa;+
Nilikujibu kutoka katika wingu lenye ngurumo.+
Nilikujaribu katika maji ya Meriba.+ (Sela)
 8 Sikieni, watu wangu, nami nitatoa ushahidi dhidi yenu.
Ee Israeli, laiti ungenisikiliza.+
 9 Hakutakuwa na mungu yeyote wa kigeni miongoni mwenu;
Nanyi hamtamwinamia mungu wa kigeni.+
10 Mimi, Yehova, ni Mungu wako,
Niliyekutoa nchini Misri.+
Fungua wazi kinywa chako, nami nitakijaza.+
11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu;
Israeli hakujitiisha kwangu.+
12 Kwa hiyo nikawaacha wafuate mioyo yao mikaidi;
Walitenda mambo waliyofikiri yanafaa.+
13 Laiti watu wangu wangenisikiliza,+
Laiti Israeli angetembea katika njia zangu!+
14 Ningewatiisha haraka maadui wao;
Ningeugeuza mkono wangu dhidi ya wapinzani wao.+
15 Wale wanaomchukia Yehova watajikunyata mbele zake,
Na mwisho wao utakuwa wa milele.
16 Lakini atakulisha ngano bora kabisa+
Na kukushibisha kwa asali kutoka mwambani.”+