Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g96 7/8 kur. 26-27
  • UFO—Je, Ni Wajumbe Kutoka kwa Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • UFO—Je, Ni Wajumbe Kutoka kwa Mungu?
  • Amkeni!—1996
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mpango wa Kuokoa wa Viumbe vya Kigeni
  • Mawasiliano ya Mungu na Wanadamu
  • Wakaaji wa Nje ya Dunia Hii—Kupata Jibu
    Amkeni!—1990
  • Kutoka kwa Wasomaji Wetu
    Amkeni!—1997
  • Wakaaji wa Nje ya Dunia Hii—Ndoto ya Tangu Kale
    Amkeni!—1990
  • Wakaaji wa Nje ya Dunia Hii—Wako Wapi?
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—1996
g96 7/8 kur. 26-27

Maoni ya Biblia

UFO—Je, Ni Wajumbe Kutoka kwa Mungu?

KARNE ya 20 imalizikapo na hali zilizo katika ulimwengu ziendeleapo kudhoofika, kuitikadi katika vitu vya anga visivyotambuliwa au unidentified flying objects (UFO) na abiria wavyo, viumbe vya anga ya nje, huendelea kuenea. Je, UFO ni hadithi ya kubuniwa tu, madanganyo, uwongo mtupu unaoendelezwa na watu wanaopenda kucheka uzuzu wa umma?

Wale wanaodai kuwa waliona UFO au abiria wao kutoka anga ya nje hutia ndani watu wanaoonekana kuwa timamu, wenye kutumainiwa; na hata wale wanaoamini katika wageni hao kutoka sayari nyinginezo watia ndani maprofesa na wanasayansi wenye elimu nyingi. Wao wamesadiki kwamba viumbe kutoka anga ya nje wanatazama wanadamu na, nyakati nyingine, kuwasiliana nao. Vile viitwavyo eti vikundi vya kutegemeza wale walioona viumbe kutoka anga ya nje viko ili kusaidia watu wanaodai kuwa wamewasiliana na wageni hao kutoka anga ya nje.a

Mpango wa Kuokoa wa Viumbe vya Kigeni

Katika kitabu Aliens Among Us, Ruth Montgomery ahoji baadhi ya watu wanaozidi kuongezeka ambao wamesadiki kwamba wao ni wageni kutoka anga ya nje ambao wanaishi katika miili ya kibinadamu. Baadhi ya wale wanaodai kuwa viumbe vya anga ya nje waliotwaa miili ya wanadamu hutabiri kwamba katika mwaka wa 2000, kutakuwa na “tukio la ulimwenguni pote ambalo kwalo wakuu wa malaika na mabwana-wakubwa wenyewe wamekuwa wakijitayarishia.” Watu wengine huamini kwamba baadhi ya viumbe kutoka anga ya nje wanatumia UFO ili kukusanya na kuhifadhi aina za mimea na wanyama au kwamba UFO zitatumiwa zikiwa vyombo vya angani vya kuokoa na kusafirisha mamilioni ya wanadamu kutoka kwenye uharibifu unaokaribia kupata dunia. Baada ya uharibifu mkubwa, wanadamu watarudishwa duniani ili kuanza “Enzi Mpya na Utaratibu Mpya” wa ufahamu wa kiroho. Kijana mmoja kutoka Colorado, Marekani, ambaye ni mshiriki wa kikundi kinachojiita “Vijana Kutoka Anga ya Nje,” aliliambia Amkeni! hivi kwa unyoofu kabisa: “Rafiki zangu pamoja na mimi tunangoja wazazi wetu wa kale wa anga ya nje watusafirishe.”

Wachache kati ya wale wanaodai kwamba wao ni viumbe kutoka anga ya nje wanadai kwamba wanaongozwa na Mungu, na wengine wanadai kwamba wao husema kwa uhuru naye wakitafuta shauri la kusaidia nalo wanadamu. Je, Mungu anatumia wageni kutoka sayari nyinginezo ili kuokoa wanadamu kutoka kwa msiba wa ulimwenguni pote unaokuja?

Mawasiliano ya Mungu na Wanadamu

Mapema katika historia, Mungu aliwasiliana na wanadamu. Rekodi ya Biblia yafafanua mazungumzo ya kimungu pamoja na Adamu na Hawa, Noa, Abrahamu, na wengine.b (Mwanzo 3:8-10; 6:13; 15:1) Ndoto, sauti, na maono yalitumiwa kuwasilisha mapenzi ya Mungu na hata kutokeza Biblia. Hata hivyo, baada ya Biblia kumaliza kuandikwa, je, kulikuwa na uhitaji wa mawasiliano ya moja kwa moja kutoka mbinguni? La, kwa kuwa Biblia yasema kwamba Maandiko Matakatifu hufanya “mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.” (2 Timotheo 3:17) Kulingana na Biblia, mwongozo katika nyakati hizi zenye taabu wapaswa kutoka kwa Neno la Mungu lililoandikwa. Hata hivyo, je, kuna sababu yoyote ya kuamini kwamba tungepokea mawasiliano au maagizo ya kipekee moja kwa moja kutoka kwa Mungu kupitia msemaji atokaye anga ya nje? La, kwa kuwa mtume Paulo alisema: ‘Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe.’—Wagalatia 1:8.

Ingawa madai ya wale waonwao kuwa eti viumbe vya anga ya nje huonekana kukubaliana na unabii mbalimbali wa Biblia kwamba karibuni dunia itapata mabadiliko makubwa yenye msiba, wao huonyesha njia ya kuokoka ambayo inategemea viumbe. Biblia haihimizi watu wakimbilie usalama wa vyombo vya anga vya viumbe vya anga ya nje au mahali pengine popote. Badala ya hivyo, inatuambia tutafute ulinzi katika uhusiano wenye wakfu pamoja na Mungu, ambao ni wakfu unaoonyeshwa kwa ubatizo wa maji. (1 Petro 3:21; linganisha Zaburi 91:7; Mathayo 28:19, 20; Yohana 17:3.) Na Yesu alisema kwamba “mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.”—Mathayo 24:13.

Je, si kweli kwamba maandiko haya yakazia uhusiano wa kiroho pamoja na Mungu ili kuokoka badala ya mahali halisi pa kukimbilia? Basi, badala ya kusaidia wanadamu kuokoka, hadithi juu ya ‘viumbe visivyo vya kibinadamu’ hukengeusha uangalifu wa watu kutoka kwa kile ambacho kweli Mungu anawaamuru wafanye kwa ajili ya hali-njema yao ya milele.

Ni nani awezaye kujaribu kuondosha wanadamu kutoka kwa njia ya Mungu ya wokovu, na bado adai kumwakilisha Mungu? Ed Conroy katika kitabu chake Report on Communion, asema kwamba “wachunguzi wa UFO kwa uzito wanaofahamu sayansi za saikolojia na jamii” hutia ndani ya chunguzi zao za kulinganisha za “‘wavizia vyumba vya kulala,’ mashetani, mashetani wenye makelele, mizimu, maono ya kidini, na kile ambacho kimeonwa kuwa roho waovu.” Wachunguzi wengi wa UFO na wale wanaodai kuwa viumbe kutoka anga ya nje wenye miili ya kibinadamu wasema kwamba haihitajiki kutumia chombo cha anga kusafiri. Wanasema kwamba viumbe hivyo vyaweza kusafiri bila kuonekana na kutokea mahali popote duniani bila kutumia chombo cha anga.

Biblia huonya kwamba Shetani na mashetani wake wameazimia kudanganya wanadamu. Wao wanatumia vibaya hali ya wanadamu ya kukata tamaa ili kuwatolea masuluhisho yenye kuvutia lakini yaliyo bandia. (2 Wakorintho 11:14) Hiyo ndiyo sababu Biblia hutuonya hivi: “Nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani.”—1 Timotheo 4:1.

Kwa njia iyo hiyo leo, zile zionwazo kuwa ziara na ule uonekanao kuwa mwongozo wenye kufaa kutoka kwa viumbe hivyo ni lazima ukataliwe, hata uje kwa njia gani. Wale wanaoona ni afadhali kufuata shauri la “viumbe kutoka anga ya nje” kuliko kufuata Neno la Mungu hakika wamedanganyika—kosa baya sana la kufanya katika nyakati hizi zenye hatari.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa mazungumzo juu ya UFO na maisha ya anga ya nje, ona matoleo ya Amkeni! ya Agosti 8, 1990, na Novemba 8, 1990, la Kiingereza.

b Mwandikaji wa Biblia Ezekieli alishuhudia kile ambacho watu wengine wamefikiria kuwa ni UFO. (Ezekieli, sura 1) Lakini, hiyo ilikuwa ni mojayapo maono mengi ya mfano yanayofafanuliwa na Ezekieli na manabii wengine, si mwono halisi kwa macho kama idaiwavyo katika nyakati za kisasa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki