Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w86 2/15 kur. 3-4
  • Ufunuo Ni Nini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufunuo Ni Nini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Maana Yake Hasa
  • Ufunuo—Wakati Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
  • Je, Ulimwengu Utakwisha Karibuni? Apokalipsi Ni Nini?
    Habari Zaidi
  • Apokalipsi—Je, Tuiogope Au Tuitumainie?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Kwa Nini Watu Huogopa Apokalipsi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1986
w86 2/15 kur. 3-4

Ufunuo Ni Nini?

“UFUNUO!” Ni jambo gani linalokuja akilini mwako unapolisikia neno hilo? Je, ni siku ya maangamizi? Maafa makubwa? Vita ya Ulimwengu ya Tatu? Mwisho wa ulimwengu? Ikiwa hizo ndizo fikira ulizo nazo akilini, si wewe peke yako. Sayansi na ‘ vyombo vya habari vinaonyesha wakati ujao wa mwanadamu kuwa bila matumaini mazuri. Kwa hiyo si ajabu kwamba watu wengi wanasema kwamba ufunuo utakuwa ni tukio la kuangamizwa kwa wanadamu wamalizike.

“Leo Ufunuo si jambo linaloelezwa na Biblia tu, bali umekuwa jambo linaloweza kutukia kikweli,” akaonya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Javier Perez de Cuellar katika hotuba yake ya kuwekwa cheoni. “Hakuna wakati wo wote wa maisha ya kibinadamu tumekuwa katika ukingo mwembamba kama sasa unaotenganisha maangamizi na wokovu.” Yeye alikuwa akimaanisha nini? Pambano la kutumia silaha za nyukilia lenye kutokezwa na ongezeko kubwa la mashindano ya kuzidisha silaha. Akikazia onyo alilotolea Umoja wa Mataifa, alisema kwamba “wanasayansi karibu 500,000 katika sehemu zote za ulimwengu wanatumia maarifa yao kutafuta silaha za ufundi mkubwa zaidi na zilizo hatari zaidi.”

Wengine, pia, wanaijua hali iliyopo leo. Hans Jonas, profesa aliyestaafu wa falsafa kwenye Shule Mpya ya Uchunguzi wa Mambo ya Kijamii, anasema kwamba woga wake mkuu ni “ufunuo unaotisha kutokea kutokana na kani zisizokusudiwa za ustaarabu wa kiufundi.”

Yeye anakamatanisha ufunuo na ‘kumalizwa, kuchafuliwa, kuachwa ukiwa kwa sayari hii, na pia tisho la uharibifu wa ghafula wenye kuletwa na kombora la atomi.’ Vivyo hivyo, mwanahistoria Golo Mann alisema: “Hatuwezi kuwa na vita ya ulimwengu nyingine. Neno vita halifai. Twapaswa kufuta usemi ‘Vita ya Ulimwengu ya Tatu’ badala yake tuseme ufunuo au maangamizi makubwa.”​—Die Zeit, Agosti 30, 1985 cha Hamburg.

Ndiyo, mwanadamu anatambua kwamba yuko kwenye ukingo wa kujiangamiza mwenyewe. Lakini je yeye ndiye atakayeufyatusha ufunuo huo wa maangamizi? Si kulingana na Biblia, inayosema kwamba “Yehova Mungu, Mweza Yote”​—wala si mwanadamu​—ndiye ‘atakayewaharibu wale wanaoiharibu dunia.’ (Ufunuo 11:17, 18, NW) Basi, kufahamu ufunuo ni nini kulingana na maoni ya Biblia huenda kukakupa maoni tofauti, yaliyo mapya kabisa na yenye tumaini zuri.

Maana Yake Hasa

Ufunuo unaelezwa katika barua waliyoandikiwa Wathesalonike. Humo mtume Paulo anasema: “Ni haki mbele za Mungu kuwalipa mateso wale wawatesao ninyi; na kuwalipa ninyi mteswao raha pamoja na sisi; wakati wa kufunuliwa kwake Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika wa uweza wake; katika mwali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu; watakaoadhibiwa kwa maangamizi ya milele, kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa nguvu zake.”​—2 Wathesalonike 1:6-10.

Basi, ufunuo ni kufunuliwa kwa Yesu wakati wa kipindi cha “dhiki kubwa.” (Mathayo 24:21) Kulingana na kamusi ya W. E. Vine inayoitwa An Expository Dictionary of New Testament Words, neno la Kigiriki a·po·kaʹly·psis linaelekeza kwa “Bwana Yesu Kristo wakati Yeye anapokuja kutoa hukumu za Mungu.” Mahali penginepo, Biblia inautaja ufunuo huo kuwa “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi” kwenye Har–Magedoni.​—Ufunuo 16:14, 16; 19:11-21.

Ni kweli kwamba tumeona Biblia inataja “dhiki,” “kisasi,” na “adhabu” kuhusiana na ufunuo. Hata hivyo, inataja pia “raha” (“faraja,” tafsiri ya New World) kwa watu wasio na hatia ambao wamepatwa na dhiki. Neno la Mungu linatuahidi kwamba “bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo.” (Zaburi 37:10) Kwa hiyo ufunuo utaondolea wanadamu mavutano yote maovu. Huo utakuwa wakati wa badiliko kubwa lenye hali bora kwa wenye mioyo minyofu​—si tukio la kuogopwa nao.

Hivyo, badala ya kuwa maangamizi ya wote, au kumaliza uhai wote, ufunuo utakuwa utatuzi wenye uadilifu kwa matatizo ya wanadamu. Je, wazo la kuishi katika kipindi kipya​—kipindi chenye uadilifu, amani, na faraja​—halikuvutiii wewe na jamaa yako?

Lakini je, tunaukaribia ufunuo ule unaotajwa na Biblia? Ikiwa ndivyo, je, tuna njia ya kuujua wakati barabara?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki