Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w98 7/1 uku. 3
  • Mbona Watu Wanaiacha Dini?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mbona Watu Wanaiacha Dini?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Sababu Inayowafanya Wakatae Dini
  • Nani Anayependezwa na Dini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1978
  • Je! Dini Yoyote Ni Nzuri vya Kutosha?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Dini Ina Faida Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Sehemu ya 24: Sasa na milele—Mazuri ya Milele ya Dini ya Kweli
    Amkeni!—1990
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
w98 7/1 uku. 3

Mbona Watu Wanaiacha Dini?

KATIKA miaka ya katikati ya karne ya 19, lilikuwa jambo geni kabisa kwa mkazi wa Prussia (sasa kaskazini mwa Ujerumani) kusema kwamba hakuwa wa dini yoyote. Kwa hakika, kuacha tu dini mashuhuri na kujiunga na kanisa ambalo halikufuata kanuni zenye kukubalika kijumla, kungeweza kumfanya mtu asakwe na polisi. Nyakati zimebadilika kama nini!

Leo, idadi kubwa ya Wajerumani wanajiuzulu kutoka makanisani. Yaripotiwa kwamba mtu 1 kati ya 4 hudai kutokuwa wa dini yoyote. Mwelekeo uo huo waonekana Austria na Uswisi. Ikiwa washiriki ndio damu iliyo muhimu kwa uhai wa dini, basi, kama vile Reimer Gronemeyer, mwandikaji Mjerumani, alivyosema, “makanisa ya Ulaya yanavuja damu nyingi kiasi cha kufa.”

Sababu Inayowafanya Wakatae Dini

Kwa nini watu wengi hukataa mashirika ya kidini? Mara nyingi, ni kwa sababu za kifedha, hasa katika nchi ambamo washiriki wanapaswa kulipa kodi ya kanisa. Watu wengi huuliza, ‘Kwa nini fedha zangu zilizochumwa kwa jasho ziliendee kanisa?’ Wengine huzuiwa na utajiri na uwezo mwingi wa kanisa. Yaelekea wao hukubaliana na Kadinali Joachim Meisner wa Cologne, Ujerumani, aliyesema kwamba huenda utajiri wa kanisa ukawa umechochea kanisa kukaza uangalifu mwingi mno kwenye mambo ya kimwili na “kuichukua imani katika Kristo hivihivi tu.”

Wengine wanaliacha kanisa lao kwa sababu lachosha, halipendezi, na haliwezi kutosheleza njaa yao ya kiroho. Wanapatwa na njaa kali iliyotabiriwa na nabii Amosi, “si njaa ya kukosa chakula, wala kiu ya kukosa maji, bali ya kukosa kuyasikia maneno ya BWANA.” (Amosi 8:11) Kwa kuwa wanapokea chakula kidogo sana cha kiroho kutoka katika dini yao, wanaiacha.

Ingawa matatizo yanayokumba watu ni halisi, je, kuiacha dini ndilo jambo linalofaa? Mwazie mtu mwenye njaa aonaye kitu kinachofanana na mkate. Hata hivyo, anapojaribu kuula, anakuta kwamba umetengenezwa kwa unga wa mbao. Je, angeacha wazo la kula na kutosheleza njaa yake? La, angetafuta chakula halisi. Vivyo hivyo, ikiwa dini fulani haitoshelezi njaa ya kiroho ya washiriki wake, je, waache dini? Au lingekuwa jambo la hekima zaidi ikiwa wangetafuta njia ya kutosheleza njaa yao ya kiroho? Hivyo ndivyo watu wengi wamefanya, kama vile makala ifuatayo ionyeshavyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki