Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 6
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyochaguliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Kazia yale matangazo yanayohitaji kuelekezewa fikira mapema, kama vile tarehe za mkusanyiko, toleo la fasihi la mwezi na kuagiza Kitabu cha Mwaka. Zungumzia mambo ya kuongelewa katika magazeti ya karibuni. Toa wonyesho kwa ufupi kuhusu matoaji ya magazeti ambayo yanaweza kutumiwa katika utumishi wa shambani juma hili.
Dak. 15: “New World Translation Yasaidia Watafutaji Ufalme.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Unaweza kukazia fikira kwenye mambo yenye msaada katika kitabu Reasoning na habari zinazopatikana katika Insight. Wakati wa kuzungumza fungu 5, wonyesho mfupi utolewe na mhubiri ambaye anaweza kutumia marejezo kutoka kitabu Reasoning wakati anapotoa Biblia.
Dak. 20: “Kwa Nini Ujifunze Biblia?” Utoaji wa Kichwa cha Mazungumzo kipya. Maelezo mafupi ya utangulizi yakiwatia wote moyo mkuu wajifunze na kutumia kichwa kipya mara moja pamoja na toleo la mwezi huu. Kazia uhitaji wa kujitayarisha na umaana wa kuwa na vipindi vya kufanya mazoezi katika jamaa. Kisha mhubiri mwenye uwezo, aliyejitayarisha vizuri atoe utoaji unaofuata ulio kiolezo:
“Watu wengi tunaozungumza nao wanapenda Biblia na wanaikubali kuwa Neno la Mungu. Hata hivyo, ingawa makao mengi yana Biblia, watu wengi hawaisomi. Kwa nini sisi tunaoishi katika karne ya 20 tunapaswa kusoma na hata kujifunza Biblia? Leo, tutazungumzia sababu mbili za msingi. Kwanza, Neno la Mungu ni lenye manufaa kweli kweli na lenye msaada kama inavyotaarifiwa hapa kwenye 2 Timotheo 3:16, 17. (Soma.) Angalia kwamba tukitumia kanuni za Biblia tutapata madokezo yenye mafaa yenye kutumika, kwa kielelezo, juu ya jinsi ya kunyoosha mambo, au kutatua matatizo, labda katika jamaa, tukiwa pamoja na marafiki au watu wengine wa ukoo, au hata mahali petu pa kazi au shuleni. Je! wewe hukubali kwamba ni jambo lenye manufaa kujua jinsi ya kutatua tofauti zinapotokea? Hakika hekima hiyo ingetusaidia tudumishe mahusiano yenye kuamanika na mema pamoja na wengine, sivyo? (Ruhusu majibu kwa maswali.) Kwa kweli Biblia inaweza kutusaidia tufanye hivyo. Sababu ya pili ya kujifunza Biblia ni kwamba inaweza pia kutusaidia tustahili kupata uhai wa milele katika paradiso hapa hapa duniani. Inawezekanaje? Angalia maneno haya kwenye Yohana 17:3. (Soma.) Na ni jambo gani linalotiwa ndani katika maarifa haya? Mistari michache kwenye Yohana 17:26 tunasoma yale ambayo Yesu alisema. (Soma.) Kwa hiyo, kama Yesu alivyoonyesha wazi angalau mtu angejua jina la Mungu na linalomaanisha. Umaana wa uhakika huu unaonyeshwa katika broshua hii: Jina la Mungu Litakaloendelea Milele. Kwenye kurasa 4, 5 tunaona jina hilo ni jina gani kama linavyofunuliwa katika Biblia. (Elekeza fikira kwenye fungu la kwanza kwenye ukurasa wa 5.) Kisha kwenye kurasa 28 na 30 kuna kichwa hiki kinachopendeza ‘Kwa Nini Ni Lazima Tujue Jina la Mungu’ na ‘Jinsi Linavyokuhusu Wewe.’” Toleo la broshua na New World Translation linaweza kufanywa kwa mchango wa kawaida. Hata toleo la fasihi likikataliwa unaweza kutoa funzo la nyumbani la Biblia la bure na kueleza utaratibu unaofuatwa.
Wimbo 98 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 13
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Tia ndani maelezo yenye kutia moyo mkuu kuhusu shukrani za Sosaiti kwa michango. Eleza mipango ya utumishi wa shambani wa mwisho-juma.
Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Kusaidiana Kuanzisha Mafunzo ya Biblia.” Maswali na majibu. Soma mafungu yote. Tia ndani wonyesho wa kumtolea mtu funzo la Biblia katika ziara ya kwanza. Tunaweza kutumia kielelezo kinachotolewa chini ya “Mafunzo ya Biblia ya Nyumbani” (Home Bible Studies) kwenye ukurasa 12 wa kitabu Reasoning.
Dak. 15: “Je! Wewe Unaitikia Njia za Mungu za Haki?” Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Machi 1, 1989, kurasa 27-9, mafungu 13-23, ikikazia uhitaji wa kuwa na mtazamo chanya na wenye kupiga moyo konde ili tushiriki kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi kwa ukamili ijapokuwa uovu unaoongezeka na udhalimu.
Wimbo 213 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 20
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Sanduku la Swali. Eleza mipango kwa ajili ya utumishi wa shambani kwa mwisho-juma huu na kuwatia wote moyo mkuu washiriki.
Dak. 15: Hotuba yenye idili ikitolewa na mzee anayestahili juu ya kichwa “Kupanga Kimbele.” Msingi wa hotuba unapatikana katika toleo la Mnara wa Mlinzi Machi 15, 1979 kurasa 16, 17, chini ya kichwa “Usivutwe na Mambo Mengine.” Kazia kupanga mambo inavyofaa na ‘kutopanga kimbele kwa ajili ya tamaa za mnofu.’—Rum. 13:14, NW.
Dak. 20: “Kupanga Kimbele Kwa Ajili ya Desemba.” Mazungumzo ya maswali kwa majibu. Katika fungu la 5, hoji mmoja au wawili ambao wametumia madokezo fulani ambayo yamefanywa katika makala. Toa wonyesho kuhusu jinsi painia mwenye ujuzi anavyoweza kusaidia mhubiri mwenye bidii atengeneze ratiba ya kibinafsi ya kupainia Desemba huu.
Wimbo 123 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA NOVEMBA 27
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Onyesha utoaji unaofaa wa magazeti ya karibuni.
Dak. 15: “Kutanguliza Masilahi za Ufalme Kwanza.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu yakifanywa na mzee anayestahili. Soma mafungu kadiri wakati unavyoruhusu.
Dak. 20: Amsha Upendezi kwa Ajili ya Ziara za Wakati Ujao. Hotuba na maonyesho. Ni jambo la maana tuwe wenye busara na wenye fadhili katika huduma yetu. (1 Kor. 9:19-23) Kuacha maono yenye kupendeleka kunaweza kuwezesha mhubiri atakayefuata atoe ushahidi kwa njia kamili zaidi. Kwa kuzusha swali tuondokapo mlangoni, tunaweza kuamsha kuwaza kwa mwenye nyumba hivi kwamba atazamie ziara inayofuata. Huenda hata akataka kuendeleza mazungumzo ya kisasa tukiuliza swali kuhusu habari fulani ambayo inampendeza. Lingekuwa jambo linalofaa kutumia habari zinazopatikana katika kitabu Reasoning katika Vichwa vya Mazungumzo. Maswali kama vile “Je! mwanadamu aliumbwa na Mungu ili afe?” (rs uku. 98), “Je! Dunia sayari itaharibiwa katika vita ya nyukilia?” (rs uku. 112, tdSW 6C), “Kusudi la uhai wa kibinadamu ni nini?” (rs uku. 243), “Mtu anaweza kujuaje dini iliyo sawa?” (rs uku 328, tdSW 5B), na “Kwa nini kuna uovu mwingi sana?” (rs uku. 427) au nyingine yoyote ambayo inaweza kufaa mahali pa kwenu inaweza kuchaguliwa kutoka kitabu Reasoning. Toa wonyesho wa kumalizia ziara mahali ambapo kupendezwa hakukuonyeshwa. Mhubiri aondokapo auliza swali akitaja kwamba angeterema kurudi wakati mwingine ili alijibu. Pia, toa wonyesho unaoonyesha jinsi mhubiri anavyoweza kutumia kitabu Reasoning kutoa jibu wakati mwenye nyumba anapoomba jibu. Mwenyekiti amalizia kwa kutoa maelezo juu ya uhitaji wa kutumia maswali yenye kumfanya mtu afikiri.
Wimbo 129 na sala ya kumalizia.