Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA MACHI 5
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yanayofaa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Sifu akina ndugu kwa uchangamfu ambao tayari wameshiriki katika huduma ya shambani mwezi huu, na uwatie moyo wote washiriki kwa bidii shambani wakati wa Machi. Toa madokezo yenye kutumika ya kutoa magazeti ya karibuni katika eneo lenu. Wakumbushe wahubiri juu ya mipango ya kundi kwa ajili ya utumishi wa shambani.
Dak. 20: “Jenga Imani Katika Neno la Mungu.” Maswali na majibu. Wakati wa kuzungumza fungu 3, wahubiri wenye matokeo kati ya waskilizaji watoe madokezo na maelezo hususa juu ya mazungumzo ya kuongea yanayoweza kutumiwa katika utumishi wa shambani. Maelezo hayo yatayarishwe kimbele.
Dak. 15: Zuru Tena ili Kuchochea Kupendezwa Zaidi. Watie moyo wahubiri wafanye ziara za kurudia mara moja kwa wote walioonyesha kupendezwa katika kitabu God’s Word. Sehemu iliyotangulia ilitaja uhitaji wa kufanya ziara za kurudia na kuanzisha mafunzo ya Biblia pamoja na watu wanaopendezwa. Baada ya mazungumzo mafupi juu ya uhitaji na kitia moyo cha uchangamfu kwa wote kurudi tena mahali ambako kupendezwa kunaonyeshwa, toa wonyesho mfupi mmoja au mawili yakionyesha jinsi ya kufanya ziara ya kurudia mahali ambako kitabu kiliangushwa.
Wimbo 23 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA MACHI 12
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu, kutia ndani shukrani kutoka kwa Sosaiti za michango yoyote iliyopelekwa wakati wa Februari. Sifu kundi kwa shauku kwa ajili ya utegemezo wa ukarimu wa kazi ya Ufalme kupitia michango yao ya kifedha. Pitia mipango ya kundi ya utumishi wa shambani, na utie moyo wahubiri wafanye kazi pamoja na vikundi vyao vya utumishi kwenye mwisho-juma. Kumbusha kundi kwamba hotuba ya peupe ya pekee itatolewa mnamo Machi 25. Rejeza kwenye tangazo katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Januari 1990.
Dak. 15: “Vitolewaji Vipya Vyatusaidia Sisi Kujizoeza Ujitoaji Kimungu.” Hotuba yenye shauku ikitia moyo wote wazoeleane kabisa na vitolewaji vipya. Waweza kutia ndani usemi mmoja mfupi au mbili uliochaguliwa wa uthamini kutoka kwa akina ndugu ambao wamesoma na kutumia vichapo.
Dak. 20: “Kutangaza Habari Njema—Kwa Kutumia Ufahamu.” Maswali na majibu. Baada ya kuzungumza fungu la 3, kuwe maonyesho mawili mafupi yakionyesha jinsi ya kurekebisha mahubiri yalingane na mastakimu za mwenye nyumba. Maonyesho yaweza kumalizwa hilo likiisha timizwa, kwa kawaida wakati wa utangulizi au mara tu baadaye.
Wimbo 225 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA MACHI 19
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia ndani mipango kwa ajili ya utumishi wa shambani wa mwisho-juma. Toa madokezo kuhusu makala katika magazeti ya karibuni zinazoweza kuvutia hasa watu katika eneo la kwenu.
Dak. 20: “Wakati wa Utendaji Ulioongezwa.” Mazungumzo ya makala kwa maswali na majibu. Taja hesabu ya wale tayari wamejiandikisha kuwa mapainia wasaidizi kwa ajili ya Aprili na Mei. Wakati wa kuzungumza fungu la 5, rejeza kwenye makala ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Februari 1990 “Magazeti Maarufu Yatokezwa.” Kwa ufupi pitia mambo ya kuzungumzia katika toleo la Mnara wa Mlinzi wa Aprili 1 ikiwa limekwisha pokewa. Watie moyo wote kwa uchangamfu wafikirie uwezekano wa kuongeza utendaji wa shambani kwa kukamatana na mpango wa hotuba ya pekee na sherehe ya Ukumbusho na pia kwa ajili ya kipindi chote cha miezi miwili.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu au hotuba na wonyesho vikikazia ubora wa kuchunguza kwa ukawaida andiko na maelezo ya kila siku. Dokeza jinsi hilo linavyoweza kufanywa. Tegemeza hotuba kwenye habari katika utangulizi wa Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—1990.
Wimbo 46 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA MACHI 26
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Watie moyo wote wanaoweza washiriki katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu. Jumapili ni siku ya kwanza ya Aprili na mwanzo wa toleo la andikisho la Mnara wa Mlinzi. Wote watakaokuwa mapainia wasaidizi wakati wa Aprili wapaswa kuwa wamekwisha peana maombi, ambayo yanapatikana kutoka kwa mwangalizi msimamzi. Kwa kadiri wakati unavyoruhusu, dokeza mahubiri yanayofaa kwa ajili ya magazeti ya karibuni.
Dak. 20: “Kuendeleza Huduma Yetu Bila Kuacha.” Maswali na majibu. Ndugu mwenye uwezo asome mafungu. Wengine katika wasikilizaji waweza kusoma na kutoa maelezo juu ya maandiko yaliyotajwa. Onyesha matumizi ya mahali penu ya habari hiyo, ukiwasaidia wahubiri wakabiliane na matatizo yanayoelekewa katika eneo na kudumisha mtazamo unaofaa. Wote wapaswa kuazimia kutumikia Yehova kwa bidii hadi mwisho wenyewe.
Dak. 15: Toa Andikisho la Mnara wa Mlinzi. Kwa ufupi zungumza juu ya umaana wa andikisho la Mnara wa Mlinzi kwa ajili ya wote ambao ni watafuta uhai katika ulimwengu mpya wa Yehova. Toa wonyesho wa toleo la andikisho. Wakati wa kutumia matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi, wahubiri waweza kujitahidi kusisimua kupendezwa kwa kutaja kwamba watu wengi leo wana wasiwasi na wamevurugika kuona dini nyingi sana zenye kupingana. Mathayo 7:13, 14 yaweza kutumiwa kuonyesha jinsi Yesu alivyodokeza kwamba si dini zote zingekubalika kwa Mungu. Dini inayompendeza Mungu haina migawanyiko na mapigano kama inavyoonyeshwa kwenye Waefeso 4:5, 13 na huhimiza kuishi kulingana na viwango vya uadilifu vya Mungu. (Tito 1:16) Wakati ukiruhusu, pia toa wonyesho wa utoaji wa andikisho ulio mfupi na wa moja kwa moja.
Wimbo 71 na sala ya kumalizia.