Mikutano Inayotusaidia Kufanya Wanafunzi
JUMA LINALOANZA AGOSTI 5
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Dokeza toleo moja au mawili ya magazeti yanayoweza kufaa eneo lenu, na kutia moyo wahubiri wote watoke nje kwa utumishi wa shambani mwishoni mwa juma hili. Leteni kitabu Kutoa Sababu kwenye Mkutano wa Utumishi juma lijalo.
Dak. 20: “Lisifu Jina la Mungu Kikamili.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Malizia kwa wonyesho uliotayarishwa vizuri kuonyesha jinsi Kichwa cha Mazungumzo cha sasa kinavyoweza kutumiwa. Tumieni Utoaji uliodokezwa katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai 1991, ukurasa wa 2.
Dak. 15: “Kupanda na Kutia Maji—Hatua za Kuelekea Kufanya Wanafunzi.” Zungumza pamoja na wasikilizaji mafungu 1-9 ya nyongeza, ukurasa wa 3. Wakati wa kuzungumzia mafungu 7-9, onyesha matumizi yenye kufaidi ya habari kwa mahoji mafupi sana ya wahubiri ambao wameweza kufanya yaliyotajwa au mambo yaliyoonwa katika kundi lenu ambayo hutoa vielezi vya mambo makuu. Hakikisha kwamba mahoji au mambo yaliyoonwa ni mafupi na yenye kueleza mambo makuu.
Wimbo 130 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA AGOSTI 12
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu. Soma shukrani kutoka kwa Sosaiti kwa ajili ya michango iliyopelekwa. Pia lipongeze kundi kwa ajili ya michango ya kutegemeza kundi lenu. Watie moyo wote washiriki katika utendaji wa utumishi wa shambani katika mwisho wa juma na nyakati nyinginezo kunapokuwa na mipango ya kutoa ushahidi wa kikundi.
Dak. 15: “Uwe Mwenye Nafsi Yote Katika Huduma ya Shambani—Sehemu ya 2.” Hotuba yenye kutia moyo na kufundisha ikizungumza habari katika makala na kutoa kielezi cha jinsi ya kutumia kitabu Kutoa Sababu. Si lazima kuwa na wengine wakitoa wonyesho wa mambo yaliyotajwa, lakini mnenaji aweza kuonyesha tu jinsi ya kupata na kutumia habari katika kifaa hiki kizuri cha utumishi wa shambani. Uwe na wonyesho mfupi kuonyesha thamani ya vipindi vya mazoezi katika kujitayarishia huduma ya shambani. Wakati ukiruhusu, waweza kumwalika mhubiri aeleze jinsi yeye hufanya hivyo.
Dak. 20: “Kupanda na Kutia Maji—Hatua za Kuelekea Kufanya Wanafunzi.” Baada ya utangulizi mfupi ili kuunganisha na habari iliyozungumzwa juma lililopita, ongoza pitio kwa maswali na majibu la mafungu 10-20 ya nyongeza, kurasa 3 na 4. Huenda baadhi ya wahubiri wakaweza kusimulia jinsi wamefanyia huduma yao maendeleo na kuanza mafunzo ya Biblia kupitia matumizi ya madokezo yaliyotolewa katika matoleo ya wakati uliopita ya Huduma ya Ufalme Yetu.
Wimbo 48 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA AGOSTI 19
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Kikumbusha. Habari za Kitheokrasi. Kadiri wakati iruhusuvyo, dokeza ni makala zipi katika magazeti ya karibuni zaweza kufaa zaidi kutolewa nyumba kwa nyumba mwishoni mwa juma hili. Tia ndani wonyesho mfupi.
Dak. 20: “Kutoa Habari Njema—Katika Eneo Lenye Kufanyiwa Kazi Mara Nyingi.” Mazungumzo ya maswali na majibu. Onyesha matumizi ya kwenu au uifanye ifae mahitaji ya kundi.
Dak. 15: “Mpango wa Funzo la Kitabu la Kundi—Sehemu ya 2.” Hotuba yenye kutia moyo ikitolewa na kiongozi wa Funzo la kitabu mwenye mafanikio.
Wimbo 25 na sala ya kumalizia.
JUMA LINALOANZA AGOSTI 26
Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Mazungumzo ya kamili juu ya mipango ya kundi ya utumishi wa shambani na mambo yanayofanywa ili kuandaa kitia-moyo na usaidizi kwa wahubiri mapainia. Fikiria hususa mahitaji ya wale ambao huenda wakawa wanaanza utumishi wao wa painia Septemba 1. Tia moyo ushiriki wa utumishi wa shambani mwishoni mwa juma hili, na kuwakumbusha wahubiri wajipatie kiasi fulani cha kitabu Creation au Kitabu Changu au Kuishi Milele ili kuvitumia katika utumishi wa shambani kuanzia Jumapili, Septemba 1.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu. Mwaweza kutumia habari katika makala ya jalada ya Juni 8, 1991, Awake! kuwa msingi wa mazungumzo au hotuba juu ya kichwa cha habari porojo.
Dak. 15: “Je! Wewe Ungali Mtumwa wa Mapokeo Yasiyo ya Kikristo?—Tohara na ‘Utakaso.’” Hotuba ikitolewa na mzee pamoja na ushiriki fulani wa wasikilizaji. Zungumza mafungu 10-16, 56 katika mfululizo juu ya Mapokeo katika Huduma ya Ufalme Yetu iliyochapwa katika 1975. Tumia maswali yaliyochapwa kukazia mambo makuu.
Wimbo 16 na sala ya kumalizia.