Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 11/93 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Novemba 1
  • Juma Linaloanza Novemba 8
  • Juma Linaloanza Novemba 15
  • Juma Linaloanza Novemba 22
  • Juma Linaloanza Novemba 29
Huduma Yetu ya Ufalme—1993
km 11/93 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Novemba

Juma Linaloanza Novemba 1

Wimbo 5

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Wapongeze wahubiri kwa ajili ya sehemu wanayoshiriki katika kazi ya kuhubiri Ufalme.

Dak. 10: “Ndoto,” kitabu Kutoa Sababu, kurasa 247-48. Ishughulikiwe kwa mazungumzo pamoja na mwanafunzi wa Biblia. Mwanafunzi auliza juu ya hekima ya kuongozwa na ndoto zetu. Zungumzia hatari ya kufanya hivyo, jinsi kungetufanya tunaswe na kusababu kwa kilimwengu na roho waovu. Onyesha umaana wa kuongozwa na kanuni za Neno la Mungu.

Dak. 10: Mahitaji ya kwenu au “Uwasiliano—Si Maongezi Tu.” Hotuba ikitegemea makala katika Mnara wa Mlinzi la Agosti 1, 1993, kurasa 3-8.

Dak. 15: “Thamani ya Biblia Katika Ulimwengu wa Leo.” Mazungumzo kati ya mwangalizi wa utumishi na mhubiri anayetaka kuboresha uwezo wake katika kazi ya nyumba kwa nyumba. Baada ya kuzungumzia fungu la 3, mwangalizi wa utumishi auliza mhubiri ajaribu utoaji uliodokezwa, mwangalizi wa utumishi akiwa kama mwenye nyumba. Baada ya kuzungumzia fungu la 4, mwangalizi wa utumishi ampa mhubiri utoaji uliodokezwa. Tia moyo kutaniko lisaidie watu wenye kupendezwa na wanafunzi wa Biblia kuthamini thamani ya Biblia New World Translation.

Wimbo 52 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 8

Wimbo 7

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Elekeza fikira kwenye “Mwezi wa Pekee Kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani,” na ualike wote wafikirie kwa uzito uwezekano wa kuongeza utumishi wao wa shambani katika Desemba wakiwa mapainia wasaidizi au kwa kufanya kazi na mapainia.

Dak. 15: “Kitabu Kiandaacho Mwongozo wa Kweli.” Makala yazungumziwa kwa maswali na majibu. Toa wonyesho wa ziara ya kurudia iliyoonyeshwa katika fungu la 3. Tia moyo wote wawe wenye idili juu ya thamani ifaayo ya Biblia wanapozungumza na watu katika kazi ya nyumba kwa nyumba na kufanya ziara za kurudia. Uwe na vichapo hivyo tayari na uwe na mwelekeo ufaao utoapo toleo.

Dak. 20: “Vijana—Fanyeni Moyo wa Yehova Ushangilie.” Mzee azungumzia mafungu 1-18 pamoja na wahubiri wawili au watatu wachanga waliobatizwa. Kazia manufaa ambazo vijana hupata kwa kielelezo chao chema na thamani ya makala za “Vijana Huuliza . . .” Zungumzia Maandiko kadiri wakati uruhusuvyo.

Wimbo 80 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 15

Wimbo 73

Dak. 10: Matangazo ya kwenu, kutia ndani ripoti ya hesabu na shukrani kwa upaji. Pongeza kutaniko kwa ajili ya utegemezo wa kifedha wa kutaniko la kwenu na kwa kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote. Taja juu ya mipango ya utumishi wa shambani kwa ajili ya mwisho-juma ujao.

Dak. 15: “Kushughulikia Mahitaji ya Kiroho ya Viziwi.” Maswali na majibu. Ikiwa hakuna washiriki wa kutaniko walio viziwi, kazia juu ya kutokupuuza viziwi wapatikanao katika eneo. Uwe tayari na trakti zilitolewa hivi karibuni kwa ajili ya viziwi ambazo zaweza kuagizwa kutoka kwa ofisi ya tawi.

Dak. 20: “Vijana—Fanyeni Moyo wa Yehova Ushangilie.” Mazungumzo ya maswali na majibu ya mafungu 19-33 ya nyongeza. Hoji mhubiri mmoja au wawili wachanga. Pata maelezo juu ya jinsi ambavyo kutaniko limekuwa msaada katika maendeleo yao ya kiroho.

Wimbo 90 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 22

Wimbo 74

Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Tia moyo wote washiriki kutoa ushahidi mwisho-juma huu.

Dak. 15: “Saidia Wanafunzi wa Biblia Wajitayarishe Kwa Ajili ya Funzo Lao.” Maswali na majibu. Soma mafungu kadiri wakati uruhusuvyo.

Dak. 20: “Je! Wewe Husababu kwa Kutumia Maandiko?” Mazungumzo ya maswali na majibu yakifanywa na ndugu mwenye matokeo katika kazi ya nyumba kwa nyumba na ziara za kurudia. (2 Tim. 4:2) Baada ya kufikiria fungu la 5, mwombe mhubiri mwenye matokeo katika kutumia kitabu Kutoa Sababu asimulie jinsi ambavyo yeye hukitumia katika kutoa ushahidi.

Wimbo 108 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Novemba 29

Wimbo 83

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Tia moyo wale wanaoweza wafanye upainia msaidizi wakati wa Desemba. Toa wonyesho wa utoaji wa magazeti ya karibuni, ukikazia makala iwezayo kutumiwa shambani mwisho-juma huu.

Dak. 15: “Biblia—Mwongozo Ufaao kwa Mwanadamu wa Kisasa.” Hotuba ikitolewa na kichwa cha familia ikitegemea makala katika Mnara wa Mlinzi la Mei 1, 1993. Kazia kwamba kutumia kanuni za Biblia kwaweza kuchochea hali ya familia yenye amani na upendo. Karibisha mmoja au wawili katika wasikilizaji watoe maelezo yaliyotayarishwa kuonyesha jinsi ambavyo shauri kutoka Neno la Mungu limesaidia familia au mtu binafsi.

Dak. 20: Kutumia Kitabu Mtu Mkuu Zaidi Ili Kusaidia Watu Walio Mfano wa Kondoo Katika Desemba. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Uliza maswali kama haya: Ni simulizi gani moja juu ya huduma ya Yesu au shughuli zake pamoja na wengine zilizokuvutia wewe zaidi? Kwa nini simulizi hilo lilikuvutia? Kichapo hiki kimekuwa cha thamani gani kwako? Umejifunza nini juu ya Yehova kwa kujifunza kichapo hicho? Ni jambo (mambo) gani ambalo umekazia unapokitoa? Mhubiri mwenye ujuzi atoe wonyesho wa utoaji wa kitabu. Tia moyo wote washiriki katika utumishi wa shambani Jumapili.

Wimbo 94 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki