Mikutano Ya Utumishi Kwa Desemba
Juma Linaloanza Desemba 5
Dak 12: Matangazo ya kwenu na Matangazo yafaayo kutoka kwa Huduma ya Ufalme Yetu. Onyesha makala moja au mbili zenye kutokeza ziwezazo kutolewa tunapotoa matoleo ya magazeti ya karibuni. Panga kuwe na mhubiri stadi aonyeshe utoaji, akitumia mojapo makala hizo.
Dak 15: “Fuliza Kufuatia Utendaji wa Kitheokrasi Wakati wa Desemba.” Maswali na majibu. Simulia yaliyoonwa yaliyofurahiwa na wengine wakati walipokuwa wakifanya upainia-msaidizi au kutoa ushahidi kivivi-hivi.
Dak 18: “Alika Wengine Wamfuate Yule Mtu Mkuu Zaidi.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Panga kuwe na maonyesho mawili mafupi. Kazia uhitaji wa kuweka rekodi zilizo sahihi za nyumba kwa nyumba; pitia kifupi habari inayopasa kurekodiwa.
Wimbo 153 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 12
Dak 13: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Ripoti ya hesabu, kutia na shukrani zozote za upaji wa hiari. Toa madokezo fulani juu ya jinsi ya kuitikia salamu za sikukuu za kilimwengu.—Ona Huduma ya Ufalme Yetu, Desemba 1990, ukurasa 8.
Dak 14: “Kazia Uangalifu Daima Ufundishaji Wako.” Hotuba ikitolewa na mwangalizi wa shule. Pitia maagizo yanayoandamana na “Ratiba ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1995,” ukionyesha vikumbusha vyovyote vinavyohitajiwa hasa na kutaniko.
Dak 18: “Onyesha Uthamini kwa Nyumba ya Mungu.” Maswali na majibu. Toa maelezo zaidi juu ya uhitaji wa kuwahi mikutanoni.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Juni 15, 1990, kurasa 26-29.
Wimbo 99 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 19
Dak 10: Matangazo ya kwenu. Pitia mipango ya kwenu ya utumishi wa shambani wakati wa kipindi cha sikukuu inayokuja. Dokeza njia za kutoa magazeti ya karibuni katika eneo la kwenu.
Dak 15: “Kigezo cha Kufuata kwa Ukaribu.” Maswali na majibu.
Dak 20: “Wasihi Wawe Wafuasi Wake.” Zungumza pamoja na wasikilizaji. Panga kuwe na maonyesho mawili mafupi. Pendekeza kwamba wote watumie wakati fulani wa utumishi wa shambani kila juma kufanya ziara za kurudia.
Wimbo 22 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Desemba 26
Dak 5: Matangazo ya kwenu. Zungumzia “Je, Saa Zenu za Mikutano Zitabadilika?” ikiwa yatumika kwa kutaniko lenu.
Dak 20: “Kufuata Sana Viwango vya Uadilifu vya Yehova.” Hotuba ikitolewa na mwangalizi-msimamizi ikitegemea kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, sura ya 11.
Dak 10: Mahitaji ya kwenu. Au toa hotuba juu ya makala “Je, Unamsaidia Mtoto Wako Kumchagua Yehova?” Katika Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1994, kurasa 26-30.
Dak 10: Jitayarishe kwa ajili ya toleo la Januari. Kitabu chochote chenye kurasa 192 kilichochapishwa kabla ya 1982 chaweza kutumiwa. Ikiwa kutaniko halina chochote akibani, kitabu Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje? chaweza kutolewa. Ikiwa kitabu hiki kitatumiwa kwenu, tayarisha wonyesho unaoweza kutumiwa wakati wa kutoa kitabu hicho mlangoni. Ikiwa kitabu kinginecho kitatolewa, tayarisha wonyesho mmoja au mawili yafaayo. Mawazo ya utoaji yaweza kupatikana katika kitabu Kutoa Sababu, kurasa 9-15. Panga kuwe na mhubiri stadi aonyeshe utoaji.
Wimbo 94 na sala ya kumalizia.