Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/98 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Juni 1
  • Juma Linaloanza Juni 8
  • Juma Linaloanza Juni 15
  • Juma Linaloanza Juni 22
  • Juma Linaloanza Juni 29
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 6/98 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Juma Linaloanza Juni 1

Wimbo 223

Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: “‘Walioandaliwa Vifaa Kikamili kwa Ajili ya Kila Kazi Njema.’” Maswali na majibu. Toa maelezo mafupi juu ya Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1989, ukurasa wa 22-24.

Dak. 22: “Kutolea Ushahidi ‘Watu wa Namna Zote.’” Mzee aelezea kwamba ijapokuwa toleo la Juni ni vitabu vyenye kurasa 192, mahali pafaapo kutolewa kitabu Mtu Mkuu au Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu kwa watu fulani, twaweza kufanya hivyo. Mzee pamoja na wahubiri kadhaa wenye uzoefu wazungumzia utoaji mbalimbali uliodokezwa. Pitia kifupi dini zilizopo kwenu, na ueleze kwa nini twapaswa kuwa na jambo fulani akilini la kuanzisha mazungumzo katika kila kisa. Panga uwe na wonyesho mmoja au mawili mafupi.

Wimbo 112 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 8

Wimbo 209

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: “Kutunza Mali za Bwana-Mkubwa.” Hotuba itolewe na mzee, ikishughulikia habari iliyo katika nyongeza.

Dak. 20: “Sisi Sote Twahitajiwa ili Kutimiza Kazi.” Maswali na majibu. Eleza kwa nini wazee hutegemea wajitoleaji wengi wenye nia ili kutimiza mambo ya lazima. Pitia mahitaji ya kwenu, kama vile kusafisha Jumba la Ufalme na kulitunza, kusaidia wagonjwa na walio wazee-wazee, na kuhubiri eneo kikamili. Waalike wazee waeleze jinsi wanavyothamini usaidizi ambao wengi hutoa kwa kupenda. Kazia jinsi jitihada ya kila mtu inavyohitajiwa zaidi.

Wimbo 153 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 15

Wimbo 7

Dak. 10: Matangazo ya kwenu.

Dak. 20: “Jikakamueni Wenyewe Kisulubu.” Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1986, ukurasa wa 10-14. Zungumzia umaana wa utumishi wa painia wa kawaida, ukitia watu moyo wajiandikishe kufikia Septemba 1.

Dak. 15: “Kutoa Ushahidi kwa Mwenendo Mzuri.” Maswali na majibu. Hoji vijana kadhaa walio kielelezo bora. Wasimulie jinsi ambavyo wengine wamevutiwa na mwenendo wao wa Kikristo. Simulia jambo moja au mawili yaliyoonwa kutoka Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 1995, ukurasa wa 24-25.

Wimbo 170 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 22

Wimbo 61

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Eleza wakati ukaguzi wa hesabu ya kutaniko ulipofanywa.

Dak. 15: Jinsi ya Kuanzisha Njia ya Kupelekea Watu Magazeti kwa Ukawaida. Onyesha kile kinachohitajiwa: Andika maangusho yote, rudi baada ya majuma mawili, eleza mawazo mapya kutoka katika magazeti ya karibuni ili kuendeleza upendezi. Tia ndani majirani, wafanyakazi wenzako, wenye duka, watumishi wa vituo vya petroli, na kadhalika. Toa maandikisho ya miezi sita kwa wale wanaoonyesha upendezi wa kuendelea. Alika mhubiri mmoja au wawili wasimulie mambo mazuri yaliyoonwa kuhusu njia ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaida.

Dak. 20: Mapainia Wasaidieni Wengine. Hotuba ikitolewa na mwangalizi wa utumishi, akipitia mipango ya kufanya mapainia wasaidie wengine kibinafsi. Eleza jinsi programu za kusaidia zilivyoanzishwa zamani. (jv-SW 100; km-SW 8/79 1, 3) Watu zaidi ya milioni moja waliobatizwa miaka mitatu iliyopita wahitaji mazoezi. Programu ya “Mapainia Wasaidia Wengine” hutumia uzoefu na mazoezi ya mapainia wa kawaida na wa pekee na wamishonari ambao wamehudhuria Shule ya Utumishi wa Painia. Mradi ni kila painia asaidie wahubiri wawili kwa mwaka wawe wenye ustadi katika huduma na kufikia kushiriki katika kiwango kikubwa. Wale wanaosaidiwa hawahitaji kuwa na wasiwasi; mkazo uko katika kitia-moyo chenye upendo, kilicho na fadhili. Programu hii mpya huandaa uwezekano wa mamia ya maelfu kuwa wahudumu wenye matokeo zaidi.

Wimbo 207 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 29

Wimbo 114

Dak. 10: Matangazo. Kumbusha wote watoe ripoti ya utumishi wa shambani ya Juni. Zungumzia toleo la fasihi la Julai.

Dak. 15: “Kupanga Kimbele kwa Ajili ya Wapendwa Wetu.” Hotuba ikitegemea Mnara wa Mlinzi, Januari 15, 1998, ukurasa wa 19-22. Onyesha hekima ya kuandika wasia na upate maelezo machache kutoka kwa wasikilizaji kuhusu manufaa za kuwa na wasia.

Dak. 20: Sisi Sote Twaweza Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi. Hotuba na mazungumzo na wasikilizaji yanayotegemea Mnara wa Mlinzi, Oktoba 15, 1987, ukurasa wa 22-27. Onyesha jinsi wale ambao wakati wao hutumiwa kwa shughuli ya kazi ya kimwili, familia au madaraka ya kibinafsi wanavyoweza kupata fursa nyingi kila siku kushiriki habari njema na wengine. Tia ndani mambo kadhaa ya kwenu yaliyoonwa.

Wimbo 76 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki