Msaidie Mwenzako Mlangoni
1. Tunanufaikaje tunapohubiri pamoja na ndugu au dada mwingine?
1 Pindi moja, Yesu aliwatuma wanafunzi 70 ili wahubiri, na ‘aliwatuma wawili-wawili.’ (Luka 10:1) Bila shaka mpango huo uliwapa wanafunzi wake fursa ya kusaidiana na kutiana moyo walipohubiri. Tunaweza kumsaidia jinsi gani mhubiri ambaye tunaandamana naye katika utumishi iwapo atahitaji msaada?
2. Kwa nini tunapaswa kusikiliza wakati mwenzetu anapozungumza na mwenye nyumba, na inafaa tufanye nini tunaposikiliza?
2 Sikiliza: Sikiliza kwa makini mwenzako anapozungumza na mwenye nyumba. (Yak. 1:19) Iwapo anasoma andiko, fungua Biblia yako na ufuatane naye. Mtazame yule anayeongea, iwe ni mwenzako au mwenye nyumba. Unaposikiliza kwa makini, huenda mwenye nyumba akachochewa kufanya vivyo hivyo.
3. Ingefaa kuchangia mazungumzo ya mwenzetu katika hali gani?
3 Tambua Wakati wa Kusema: Mhubiri mwenzetu anapoongea na mwenye nyumba, tunamheshimu kwa kumruhusu aongoze mazungumzo. (Rom. 12:10) Hatupaswi kukatiza mazungumzo. Mwenzetu akisahau jambo alilotaka kusema au akiomba tumsaidie kujibu swali au kipingamizi cha mwenye nyumba, tutajitahidi kuendeleza mazungumzo yake badala ya kuanza kuzungumzia habari tofauti. (Met. 16:23; Mhu. 3:1, 7) Ikiwa tutaamua kusema, basi maneno yetu yanapaswa kuchangia ushahidi ambao mwenzetu anatoa.—1 Kor. 14:8.
4. Ni nini kitakachochangia furaha na mafanikio yetu katika utumishi?
4 Wakati wale wanafunzi 70 walipomaliza kuhubiri, ‘walirudi wakiwa na shangwe.’ (Luka 10:17) Sisi pia tutafurahia utumishi tukisikiliza na kutambua wakati unaofaa wa kusema ili kumsaidia ndugu au dada ambaye tunaandamana naye katika utumishi.