Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/10 uku. 3
  • Msaidie Mwenzako Mlangoni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Msaidie Mwenzako Mlangoni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari Zinazolingana
  • Usiwe Mwandamani Anayenyamaza Tu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Kuboresha Ustadi Wetu Katika Huduma—Uwe Mwandamani Mzuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Kujengana Tunapokuwa Katika Huduma
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Kusaidia Wengine Tunapokuwa Katika Utumishi wa Shambani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1991
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 3/10 uku. 3

Msaidie Mwenzako Mlangoni

1. Tunanufaikaje tunapohubiri pamoja na ndugu au dada mwingine?

1 Pindi moja, Yesu aliwatuma wanafunzi 70 ili wahubiri, na ‘aliwatuma wawili-wawili.’ (Luka 10:1) Bila shaka mpango huo uliwapa wanafunzi wake fursa ya kusaidiana na kutiana moyo walipohubiri. Tunaweza kumsaidia jinsi gani mhubiri ambaye tunaandamana naye katika utumishi iwapo atahitaji msaada?

2. Kwa nini tunapaswa kusikiliza wakati mwenzetu anapozungumza na mwenye nyumba, na inafaa tufanye nini tunaposikiliza?

2 Sikiliza: Sikiliza kwa makini mwenzako anapozungumza na mwenye nyumba. (Yak. 1:19) Iwapo anasoma andiko, fungua Biblia yako na ufuatane naye. Mtazame yule anayeongea, iwe ni mwenzako au mwenye nyumba. Unaposikiliza kwa makini, huenda mwenye nyumba akachochewa kufanya vivyo hivyo.

3. Ingefaa kuchangia mazungumzo ya mwenzetu katika hali gani?

3 Tambua Wakati wa Kusema: Mhubiri mwenzetu anapoongea na mwenye nyumba, tunamheshimu kwa kumruhusu aongoze mazungumzo. (Rom. 12:10) Hatupaswi kukatiza mazungumzo. Mwenzetu akisahau jambo alilotaka kusema au akiomba tumsaidie kujibu swali au kipingamizi cha mwenye nyumba, tutajitahidi kuendeleza mazungumzo yake badala ya kuanza kuzungumzia habari tofauti. (Met. 16:23; Mhu. 3:1, 7) Ikiwa tutaamua kusema, basi maneno yetu yanapaswa kuchangia ushahidi ambao mwenzetu anatoa.—1 Kor. 14:8.

4. Ni nini kitakachochangia furaha na mafanikio yetu katika utumishi?

4 Wakati wale wanafunzi 70 walipomaliza kuhubiri, ‘walirudi wakiwa na shangwe.’ (Luka 10:17) Sisi pia tutafurahia utumishi tukisikiliza na kutambua wakati unaofaa wa kusema ili kumsaidia ndugu au dada ambaye tunaandamana naye katika utumishi.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki