Kutoka kwa Wasomaji Wetu
Kwa Nini Udhibiti Hasira? Asanteni kwa ile makala “Kwa Nini Udhibiti Hasira Yako?” (Juni 8, 1997) Nililelewa katika familia kubwa na katika utoto niliona mapigano mengi katika nyumba yetu. Wazazi wangu walitalikana, na tangu wakati huo nimekuwa na mifoko ya hasira mara kwa mara. Mchana na usiku nimesali kwa Yehova, nikimwomba anisaidie kwa tatizo hili. Ulikuwa mshangao kama nini kusoma makala hii, ambayo ilionekana kana kwamba imeelekezwa kwangu! Ninatilia maanani maandiko yaliyotajwa—kwa kielelezo, Waefeso 4:26, ambalo husema: “Msiache jua litue mkiwa katika hali ya kuchokozeka.” Mume wangu nami tumetumia hili. Asante kwa Yehova na makala hii, nimeweza kulishinda tatizo langu.
A. R. S., Marekani
Kukabiliana na Mishiko ya Hofu ya Ghafula Ni lazima nimshukuru Yehova kwa moyo wote kwa ajili ya ile makala “Kukabiliana na Mishiko ya Hofu ya Ghafula.” (Juni 8, 1996) Hivi karibuni dada yangu ameharibikiwa akili. Hatukujua ni nini lililokuwa linampata, kwani hakukuwa na daktari yeyote aliyeweza kudodosa hali yake. Mwishowe, alilazwa hospitalini, akadodoswa kuwa alikuwa ameharibikiwa akili naye alikuwa ana mishiko ya hofu ya ghafula. Makala hiyo ilikuja tu kwa wakati ufaao, ikitufanya tuhisi kwamba Yehova hutujali. Dada yangu aliketi akilia alipokuwa akiisoma, kwani wakati huo alijua kikweli kuwa Yehova alielewa kabisa alichokuwa akikabili. Maneno ya dada aliyenukuliwa kwenye makala hiyo, akisema kwamba mara nyingi alikuwa amemwona Yehova kuwa chanzo cha nguvu na faraja, huonyesha jinsi Yehova Mungu wetu alivyo wa ajabu sana.
A. E. W., Afrika Kusini
“Katika Masikio ya Kitoto” Makala hii (Juni 8, 1997) iliniathiri sana. Katika huduma ya shambani, mara nyingi mimi hukutana na wachanga. Bila kuwapuuza au kuwashusha, kila wakati mimi huzungumza nao kuhusu Paradiso. Shukrani nyingi sana kwa kuchapisha jambo hili lililoonwa, kwani lilinitia moyo niendelee katika njia hii. Nani ajuaye ni masikio ya nani yatakayokuwa “masikio ya kitoto” yafuatayo?
M. O. U., Nigeria
Makala hii iliniathiri! Nilipoifikia sehemu “Kujifunza Kweli ya Biblia” na kusoma kuhusu mshtuko ambao Louise alihisi alipoona Zaburi 37:9 kuhusu kuirithi dunia—na isitoshe katika Biblia yake ya King James Version!—nililia sana. Asanteni kwa masimulizi haya ya maisha na tafadhalini endeleeni kuyachapisha kwa ukawaida katika Amkeni!
P. C., Uingereza
Kutoka kwa Wasomaji Wetu Natunza sana magazeti yote tunayopokea. Hasa nilifurahia maelezo kutoka kwa wasomaji katika Amkeni! la Juni 8, 1997 kuhusu kutenga na ushirika. Nilitengwa na ushirika kisha nikarudishwa mwaka uliofuata. Watu wengi hufikiri kuwa hatua hii ni kali. Lakini kwa kweli si kali. Nidhamu niliyoipata ilikuwa vigumu kuikubali lakini kwa hakika haikuwa kali. Najua kwamba wazee walikuwa tu wakijaribu kunisaidia. Ilikuwa kukataa kwangu msaada wao kulikoniongoza kwenye kutengwa na ushirika. Nilipotengwa na ushirika, ndipo nilipotambua jinsi ambavyo maisha yana upweke bila Yehova. Kulikuwa na utupu mwingi katika maisha yangu ambao haungeweza kujazwa hadi nilipobadili mtindo-maisha wangu na kumrudia Yehova. Kutengwa na ushirika kulininyenyekeza na kunionyesha kwamba nilimhitaji Yehova na tengenezo lake.
A. C., Kanada
Amkeni! Mnisamehe kwa kusahau kufanya upya andikisho langu la gazeti zuri la Amkeni! Ni gazeti lenye kuarifu, la kielimu, na la mambo ya hakika lenye vichwa vyenye kuchochea na vyenye kutokeza. Ningependa kupata matoleo yote ya wakati uliopita ambayo nilikosa. Sitaki kukosa hata moja. Asanteni kwa kusaidia kwa subira kupigana na hali ya kutokuwa na ujuzi.
N. S., Sri Lanka