Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Agosti 1
“Unafikiri watu wanahitaji nini ili wawe wenye furaha? [Mruhusu ajibu, kisha usome Mathayo 5:3.] Hilo ni jambo moja tu kati ya mambo ambayo Yesu alisema kuhusu furaha. Makala hii inazungumzia mambo tunayoweza kujifunza kutoka kwa Yesu kuhusu jinsi ya kupata furaha ya kweli.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 16.
Amkeni! Agosti
“Sinema nyingi leo huonyesha mambo ya roho waovu, ulozi, na uchawi. Je, unafikiri roho waovu wako? [Mruhusu ajibu, kisha usome 1 Wakorintho 10:20.] Makala hii inaonyesha mambo ambayo Biblia inasema kuhusu roho waovu na jinsi tunavyoweza kujilinda nao.” Mwonyeshe makala inayoanzia ukurasa wa 20.
Mnara wa Mlinzi Septemba 1
Taja jambo ambalo limetangazwa katika vyombo vya habari linalowahangaisha watu katika eneo. Kisha useme: “Umewahi kujiuliza ni kwa nini watu hufanya mambo mabaya kama hayo? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatupa sababu ya kuwa na tumaini. [Soma 2 Petro 3:13.] Gazeti hili linaonyesha mambo ambayo Biblia inasema kuhusu chanzo cha uovu na jinsi Mungu atakavyokomesha matendo maovu hivi karibuni.”
Amkeni! Septemba
“Unafikiri simu za mkononi, barua pepe, vituo vya maongezi, na njia nyingine za kisasa za mawasiliano zimeondolea mbali upweke au zimeuchangia? [Mruhusu ajibu.] Ona dokezo hili la kutusaidia kuushinda upweke. [Soma Matendo 20:35.] Gazeti hili litakupa mashauri mengine mazuri kutoka katika Biblia.”