Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 10/11 uku. 2
  • Usisite

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Usisite
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Vijana—Tumieni kwa Manufaa Masomo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Shule Yenye Mafanikio Ambayo Ni ya Ulimwenguni Pote
    Amkeni!—1995
  • Umewatayarisha Watoto Wako?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Uandikishwaji Katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 10/11 uku. 2

Usisite

1. Ni nini kinachohitaji ujasiri, na kwa nini?

1 Je, umewahi kusita kutoa ushahidi shuleni kwa sababu unaogopa kudhihakiwa? Kwa kweli unahitaji kuwa na ujasiri ili uweze kueleza wengine imani yako, hasa ikiwa wewe ni mwenye haya. Ni nini kitakachokusaidia?

2. Kwa nini tunahitaji utambuzi tunapohubiri shuleni?

2 Tumia Utambuzi: Ingawa shule inaweza kuonwa kwa kufaa kuwa eneo lako la kibinafsi, kumbuka kwamba si lazima uanzishe mazungumzo ya Biblia na kila mtu kama vile ambavyo ungefanya unapohubiri nyumba kwa nyumba. Tumia utambuzi ili ujue wakati wa kuzungumza. (Mhu. 3:1, 7) Kichwa cha mazungumzo darasani au mgawo wa shule unaweza kukupa fursa ya kueleza imani yako. Au mwanafunzi mwenzako anaweza kukuuliza kwa nini hushiriki katika mambo fulani. Wakristo wengine wamewaeleza walimu wao mwanzoni mwa mwaka wa shule kuwa wao ni Mashahidi wa Yehova na kuwapa machapisho yanayoeleza imani yetu. Wengine wameacha machapisho juu ya dawati ili kuwachochea wanafunzi wenzao waulize maswali.

3. Unaweza kujitayarisha jinsi gani kutoa ushahidi shuleni?

3 Jitayarishe: Ukijitayarisha, utakuwa na uhakika zaidi. (1 Pet. 3:15) Kwa hiyo jaribu kuwazia kimbele maswali ambayo huenda yakazuka, na ufikirie jinsi ungejibu. (Met. 15:28) Ikiwezekana, beba Biblia yako na machapisho kadhaa, kama vile kitabu Kutoa Sababu,vitabu vya Vijana Huuliza na machapisho kuhusu uumbaji, ili uweze kuvirejelea inapohitajika. Uliza wazazi wako watie ndani vipindi vya mazoezi wakati wa ibada ya familia.

4. Kwa nini uendelee kutoa ushahidi shuleni?

4 Uwe na maoni yanayofaa: Usidhani kwamba nyakati zote wanafunzi wenzako watakudhihaki unapowahubiria. Yaelekea wengine watapendezwa na ujasiri wako na huenda hata wakusikilize. Lakini usivunjike moyo ikiwa hakuna atakayesikiliza. Yehova anapendezwa kwa sababu ulijaribu. (Ebr. 13:15, 16) Endelea kumwomba akusaidie ‘uendelee kusema kwa ujasiri wote.’ (Mdo. 4:29; 2 Tim. 1:7, 8) Hebu wazia furaha utakayopata ikiwa mtu fulani atasikiliza. Hatimaye, huenda mtu huyo akajiunga nawe katika kumtumikia Yehova!

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki