Utendaji wa Mashahidi wa Yehova Katika Nyakati za Kisasa
Rumania
Ili kuwavunja moyo Mashahidi wa Yehova na kuharibu tengenezo lao nchini Rumania, Shetani alitumia wapelelezi, watu waliowapasha wenye mamlaka habari, ndugu wa uwongo, na pia mambo kama vile mateso, vifungo, na kazi ngumu. Lakini jitihada zake hazikufua dafu. Soma kumhusu Ioan, aliyesali kwa sauti alipokabili kikosi cha wauaji, na Teodor, aliyeimba nyimbo za Ufalme pamoja na Mashahidi wengine huku mabomu yakiangushwa. Soma pia kuwahusu watu waliotembea bila viatu umbali wa kilometa 100 ili wahudhurie mikutano. Yamkini unataka kujua kwa nini mvulana mdogo alisema hivi kwa mshangao: “Baba, unanuka kama andiko la siku!”
Zambia
Ndugu zetu nchini Zambia walikabili marufuku na matatizo mengine mengi. Wamishonari wao walifukuzwa nchini, na wototo wao wakafukuzwa shuleni. Katika masimulizi haya utasoma kumhusu mwanafunzi msichana, aliyetetea habari njema mahakamani, mkimbizi mlemavu aliyekuwa na “mwendo wa kasi kuliko tai,” na Mwanafunzi wa Biblia aliyepigwa kiboko. Soma kuhusu gari lililoteketea, kilima cha mchwa kilicholipuliwa, na jumba la kufanyia mikutano lililofanana na farasi mweusi. Masimulizi haya yanaonyesha jinsi ndugu zetu walivyokabiliana na mbu, mbung’o, nyoka, na simba walipojitahidi kutangaza habari njema katika nchi hii ya Afrika yenye mandhari nzuri.