Ikiwa Utoaji Ni Wenye Matokeo, Utumieni!
1 Huduma Yetu ya Ufalme inatutolea kikawaida matangulizi mengi kwa ajili ya mahubiri, jambo linalotutolea mawazo mapya ili kuamsha kupendezwa kuelekea ujumbe wa Ufalme. Labda tunafanya kila mwezi jitihada za kujifunza moja au mengi ya matangulizi hayo. Hata hivyo, inawezekana wahubiri wazani kwamba wana wakati tu wa kutumia utangulizi moja mara nyingi kabla ya matangulizi mengine kutokea katika makala mpya ya Huduma Yetu ya Ufalme. Bila shaka, haiwezekani kwa wote kujifunza utangulizi mpya kabla ya kuelewa ule uliotangulia.
2 Kwa upande mwingine, maelfu ya mapainia na wahubiri wengine wanatoa wakati mwingi kwa ajili ya mahubiri. Zaidi ya hilo, hesabu ya kutosha ya makutaniko yanatembelea eneo layo kwa kipindi cha majuma machache. Katika hali kama hizo, wahubiri ni wenye furaha kuwa na njia mpya za kuwakaribia watu na mawazo mapya ili kutoa ujumbe. Hilo linawasaidia kujifanya kuwa bora. Huduma yao pia ni yenye kupendeza, yenye kuzaa matunda, na hivyo wana uwezo wa kushindana na matatizo wanayokutana nayo.
3 Kwa vyovyote, ikiwa tulitayarisha utangulizi unaowezesha kwa matokeo kuamsha kupendezwa, basi tuendelee kuutumia! Si jambo la lazima kuacha kutumia utoaji wenye kufaa ikiwa unatoa matokeo. Tuuambatanishe tu na kichapo tunachotolea mwezi huu. Huku tukirudilia madokezo ya Huduma Yetu ya Ufalme, tutoe nukta zenye kupendeza ambazo tunatamani kuingiza katika utangulizi.
4 Hivyo, wakati tunapopokea chapa mpya ya Huduma Yetu ya Ufalme, tukumbuke kwamba matangulizi yaliyochapwa ndani ni madokezo tu. Ikiwa tunaweza kuyatumia, ni vema sana. Lakini ikiwa tumekwisha kuwa na utangulizi unaotoa matokeo katika eneo letu, hivyo basi tuutumie! Jambo la lazima ni kwamba ‘tutimize kikamili huduma yetu’ kwa namna iliyo bora, tukipata wale wanaostahili na kuwasaidia wawe wanafunzi.— 2 Tim. 4:5.