Zaburi
106 Msifuni Yah!*
2 Ni nani anayeweza kutangaza kikamili matendo ya Yehova yenye nguvu
Au kutangaza matendo yake yote yanayostahili sifa?+
3 Wenye furaha ni wale wanaotenda haki,
Ambao sikuzote wanatenda yaliyo sawa.+
4 Nikumbuke, Ee Yehova, unapowaonyesha kibali* watu wako.+
Nitunze kwa matendo yako ya wokovu,
5 Ili nifurahie wema unaowaonyesha watu wako uliowachagua,+
Ili nishangilie pamoja na taifa lako,
Ili nikusifu kwa fahari* pamoja na urithi wako.
7 Mababu zetu kule Misri hawakuthamini* kazi zako zinazostaajabisha.
Hawakukumbuka upendo wako mwingi mshikamanifu,
Bali waliasi baharini, kando ya Bahari Nyekundu.+
9 Aliikemea Bahari Nyekundu, ikakauka;
Aliwaongoza katika vilindi vyake kana kwamba wanapitia jangwani;*+
10 Aliwaokoa kutoka mikononi mwa adui yao+
Na kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.+
13 Lakini walisahau haraka mambo aliyotenda;+
Hawakungojea ushauri wake.
15 Aliwapa walichoomba,
Lakini akawapiga kwa ugonjwa uliowadhoofisha.+
17 Kisha dunia ikafunguka na kummeza Dathani
Na kuwafunika wale waliokusanyika pamoja na Abiramu.+
18 Moto uliwaka katika kundi lao;
Mwali wa moto ukawateketeza kabisa waovu.+
19 Walitengeneza ndama kule Horebu
Na kuiinamia sanamu ya chuma;*+
20 Waliubadili utukufu wangu
Kwa mfano wa ng’ombe dume anayekula nyasi.+
21 Walimsahau Mungu+ Mwokozi wao,
Aliyetenda mambo makuu nchini Misri,+
22 Kazi zinazostaajabisha katika nchi ya Hamu,+
Mambo yanayoogopesha kwenye Bahari Nyekundu.+
23 Alikuwa karibu kuamuru waangamizwe,
Lakini Musa, mchaguliwa wake, akaingilia kati*
Ili kuzuia hasira yake inayoangamiza.+
26 Kwa hiyo akainua mkono wake na kuapa kuwahusu
Kwamba angewaangusha nyikani;+
27 Angewaangusha wazao wao miongoni mwa mataifa,
Naye angewatawanya katika nchi mbalimbali.+
30 Lakini Finehasi alipoinuka na kuingilia kati,
Pigo hilo lilikomeshwa.+
31 Na jambo hilo likahesabiwa kwake kuwa uadilifu
Katika vizazi vyote milele.+
33 Waliitia uchungu roho yake,
Naye akaongea bila kufikiri kwa midomo yake.+
37 Waliwatoa dhabihu wana wao
Na mabinti wao kwa roho waovu.+
38 Waliendelea kumwaga damu isiyo na hatia,+
Damu ya wana wao na mabinti wao wenyewe
Ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani;+
Na nchi ikachafuliwa kwa umwagaji wa damu.
39 Wakawa wachafu kwa sababu ya kazi zao;
Walifanya ukahaba wa kiroho kwa matendo yao.+
40 Kwa hiyo hasira ya Yehova ikawaka dhidi ya watu wake,
Naye akauchukia sana urithi wake.
42 Maadui wao waliwakandamiza,
Nao wakatiishwa chini ya nguvu zao.*
43 Aliwaokoa mara nyingi,+
Lakini walikuwa wakiasi na kukosa kutii,+
Nao walikuwa wakifedheheshwa kwa sababu ya makosa yao.+
45 Na kwa ajili yao alikuwa akikumbuka agano lake,
Naye alikuwa akiwahurumia,* akichochewa na upendo wake mwingi* mshikamanifu.+
46 Alikuwa akisababisha wahurumiwe
Na wote waliowachukua mateka.+
47 Tuokoe, Ee Yehova Mungu wetu,+
Na kutukusanya kutoka katika mataifa+
Ili tulishukuru jina lako takatifu
Na watu wote waseme, “Amina!”*
Msifuni Yah!*