Zaburi
Miktamu ya Daudi.
16 Unihifadhi, Ee Mungu, kwa maana nimekukimbilia wewe.+
2 Nimemwambia Yehova: “Wewe ni Yehova; wema wangu si kwa ajili yako,+
3 Bali kwa watakatifu walio duniani.
Wao, naam, wale mashuhuri, ndio ninaopendezwa nao kabisa.”+
4 Maumivu huwa mengi kwa wale ambao, wakati kuna mtu mwingine, humfuata haraka.+
Sitamimina matoleo yao ya kinywaji ya damu,+
Nami sitayachukua majina yao juu ya midomo yangu.+
5 Yehova ndiye sehemu ya fungu langu+ nililogawiwa na ya kikombe changu.+
Wewe unaishika sana kura yangu.
7 Nitambariki Yehova, ambaye amenipa shauri.+
Kwa kweli, nyakati za usiku figo zangu zimenirekebisha.+