Zaburi
Kwa kiongozi juu ya Yeduthuni. Ya Asafu.+ Muziki.
77 Kwa sauti yangu nitamlilia Mungu mwenyewe,+
Kwa sauti yangu kwa Mungu, naye hakika atanisikiliza.+
2 Katika siku ya taabu yangu nimemtafuta Yehova mwenyewe.+
Usiku, mkono wangu umenyooshwa wala haufi ganzi;
Nafsi yangu imekataa kufarijiwa.+
6 Nitakumbuka muziki wangu wa kinanda wakati wa usiku;+
Nitaonyesha hangaiko moyoni,+
Na roho yangu itatafuta kwa uangalifu.
8 Je, fadhili zake zenye upendo zimekoma milele?+
Je, neno lake limekuwa bure+ kwa kizazi baada ya kizazi?
9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye kuonyesha kibali,+
Au je, amezifungia rehema zake kwa hasira?+ Sela.
10 Na je, nitaendelea kusema: “Hili ndilo linalonichoma,+
Kubadilika kwa mkono wa kuume wa Aliye Juu Zaidi”?+
14 Wewe ndiye Mungu wa kweli, unayefanya kwa njia ya ajabu.+
Umezijulisha nguvu zako katikati ya vikundi vya watu.+
16 Maji yamekuona wewe, Ee Mungu,
Maji yamekuona wewe; yakaanza kuwa na maumivu makali.+
Pia, vilindi vya maji vikaanza kutetemeka.+
17 Mawingu yamemwaga maji kwa kunguruma;+
Anga lenye kutanda mawingu limetoa sauti.
Pia, mishale yako mwenyewe ilienda huku na huku.+
Dunia ikatetemeka na kuanza kutikisika.+