Muziki.
98 Mwimbieni Yehova wimbo mpya,+
Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.+
Mkono wake wa kuume, naam, mkono wake mtakatifu, umempatia wokovu.+
2 Yehova amefanya wokovu wake ujulikane;+
Ameufunua uadilifu wake machoni pa mataifa.+
3 Amezikumbuka fadhili zake zenye upendo na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.+
Miisho yote ya dunia imeuona wokovu wa Mungu wetu.+
4 Mpigieni Yehova kelele za ushindi, enyi nyote watu wa dunia.+
Changamkeni na kupiga vigelegele kwa shangwe na kupiga muziki.+
5 Mpigieni Yehova muziki kwa kinubi,+
Kwa kinubi na sauti ya muziki.+
6 Kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu+
Pigeni kelele za ushindi mbele za Mfalme, Yehova.
7 Bahari na ingurume na vyote vinavyoijaza,+
Nchi yenye kuzaa na wanaokaa humo.+
8 Mito na ipige makofi;
Milima yote pamoja na ipige vigelegele kwa shangwe+
9 Mbele za Yehova, kwa maana amekuja kuihukumu dunia.+
Ataihukumu nchi yenye kuzaa kwa uadilifu+
Na vikundi vya watu kwa unyoofu.+