1 Timotheo
2 Kwa hiyo nahimiza kwa bidii, kwanza kabisa, kwamba dua, sala, maombezi, matoleo ya shukrani, yafanywe kuhusu watu wa namna zote, 2 kuhusu wafalme na wote wale walio katika cheo cha juu; ili tupate kuendelea kuishi maisha yaliyo shwari na matulivu pamoja na ujitoaji-kimungu kamili na uchukuaji-mambo kwa uzito. 3 Hili ni bora na lenye kukubalika machoni pa Mwokozi wetu, Mungu, 4 ambaye mapenzi yake ni kwamba watu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli. 5 Kwa maana kuna Mungu mmoja, na mpatanishi mmoja kati ya Mungu na wanadamu, mwanadamu Kristo Yesu, 6 aliyejitoa mwenyewe kuwa fidia inayolingana kwa ajili ya wote—hili ndilo jambo lipaswalo kutolewa ushahidi kwenye nyakati maalumu zalo lenyewe. 7 Kwa kusudi la ushahidi huo mimi niliwekwa rasmi kuwa mhubiri na mtume—ninasema kweli, sisemi uwongo—mwalimu wa mataifa kwa jambo la imani na kweli.
8 Kwa hiyo nataka kwamba katika kila mahali wanaume waendeleze sala, wakiinua mikono yenye uaminifu-mshikamanifu, bila hasira ya kisasi na mashindano ya maneno. 9 Hivyohivyo natamani wanawake wajirembe wenyewe katika mavazi yenye mpangilio mzuri, pamoja na kiasi na utimamu wa akili, si kwa mitindo ya kusuka nywele na dhahabu au lulu au mvao ulio ghali sana, 10 bali katika njia inayofaa wanawake wanaodai kumstahi Mungu, yaani, kupitia kazi zilizo njema.
11 Acha mwanamke ajifunze akiwa kimya na kwa unyenyekeo kamili. 12 Mimi siruhusu mwanamke kufundisha, wala kutumia mamlaka juu ya mwanamume, bali kuwa kimya. 13 Kwa maana Adamu alifanyizwa kwanza, kisha Hawa. 14 Pia, Adamu hakudanganywa, bali mwanamke alidanganywa kabisa akaja kuwa katika ukiukaji-sheria. 15 Hata hivyo, mwanamke atatunzwa salama kupitia uzaaji-watoto, mradi wao waendelea katika imani na upendo na utakaso pamoja na utimamu wa akili.